Monday 7 November 2016

KUELEKEA UCHAGUZI MKUU MAREKANI

UMOJA WA MATAIFA ULIPONICHANIA MKEKA WA “PERFECT COMBO” YA SAUTI NYORORO VS WAPINGA UMAGHARIBI

Na
PETER MMBAGA
+255 656 859 045.


 Kuna mwalimu wangu kwa jina la Emmanuel Maqway, nina sababu za mimi kujivunia tafakuri hii aliwahi kutusisitizia kiujumla wanafunzi wake kuwa usipokuwa mwanaminifu kwa vitu vidogo vidogo  hata vikubwa ni tatizo, sasa katika vitu vidogo wamefanikiwa, uwezo, utekelezaji  na wana misimamo ya aina yake!
Nimemkumbuka Delilah kwenye Biblia, wasomaji biblia mtanielewa hapa zaidi, kipindi mamia ya mijianaume ya kifilisti iliposhindwa kupambana na Samson, ikamtumia  mwanamke kumwangusha mwamba. Fikiria mwanamke mmoja tu!
Kisa cha kanisa la Anglikana kuanzishwa, ilikuwaje?Mwaka 1527, Mfalme Henry VIII  wa Uingereza aliwaza penzi la Anne Boleyn aliyekuwa  msaidizi wa mkewe Catherine wa Aragon na  kutaka kumuoa, kanisa Katoliki likaweka pingamizi kwakuwa talaka haruhusiwi, Henry VIII akaona dola kubwa ya Uingereza haiwezi ingiliwa na dola ya Roma, akajitoa rasmi ndani ya ukatoliki na kuupiga marufuku Uingereza. Mfalme Henry VIII akampa mkewe talaka na akawa kiongozi mkuu wa kanisa la Anglikana. Twende taratibu utanielewa, nguvu ya mwanamama hiyo!
Hata dola ya Israeli kugawanyika kusini na kaskazini moja ya sababu ni  matokeo ya mfalme Suleimani kuwa na “masuria”  ubavuni  mwake walitokea Misri waliomletea miungu ya Baali  kipindi cha malkia wa Sheba akamuasi Mungu   wa kweli! “Masuria” hao?
Maajabu ya wanawake ni wavumilivu, jasiri, na uwezo wa hali ya juu sana ila ni watu wa kupenda  ushauri, kujaliwa na kusikilizwa, usiyafanye yote hayo na  usiombe achoke, akasirike na yamfike, utajuta!  Utajua yeye ni mwanamke, kiumbe chenye nguvu!
Dunia ina mambo ila wanadamu wana mambo ya ajabu, na ukistaajabu ya Musa, utayaona ya firauni, haitii shaka unapoona  kuhusu kisichotarajiwa kabisa lakini kuna wanaojua kabisa kitatukia. Twende taratibu, utanielewa!
Kuna jamaa anaitwa Pablo Reyes pale Marekani kashajijengea umaarufu kwa alichokiandika desemba mwaka jana kupitia  ukurasa wake wa facebook, kuwa  mwaka 2016 tulioko sasa, kuna vifo vya watu maarufu duniani  kama mpiganaji wa mtaani, Kimbo Slice, mwanamuziki mwingereza Prince, mwanandondi Muhammad Ali, Gorilla, na nchi ya Marekani itashuhudia mauaji ya kinyama(mfano mdogo, polisi na watu weusi), vyote hivyo vimeshatokea. Utabiri umetimia!
Kwa maelezo yake kilichobaki ni kifo cha Donald Trump, mgombea urais Marekani kupitia chama cha Republican na mwanamama Hillary Clinton, mgombea kupitia chama cha Democratic  kuwa rais wa kwanza mwanamke nchini Marekani, utabiri wake utatimia? 
Mgombea urais Marekani kwa chama cha Democratic, Mama Hillary Clinton.
Unajua Wamarekani kesho Jumanne ya novemba 8,  wanaamua nani awe Rais?, na Pablo alipotaja mwanamama kuiongoza Marekani, ndipo jicho lilipojikita, hapohapo  Washington D.C, jirani ni shirika  la fedha duniani(IMF) kuna mwanamama  mwenye misimamo yake wa kifaransa anaitwa Christine Lagarde  anakwenda kwenye muhula wa pili  wa miaka mitano baada ya kuongoza taasisi hiyo yenye nguvu duniani toka 2011, masharti magumu yaliyobadilisha siasa za dunia ya tatu yaliletwa nao!
Bosi wa IMF, Mama Christine Lagarde.
Malkia wa Uingereza, Elizabeth II anaongoza “sakata” akimpa nguvu ya kiutendaji, Theresa May ambaye kaikamata nafasi ya Waziri Mkuu hivi karibuni , pale Ujerumani yalikwishatimia kwa kansela Angela Merkel, Anasubiri kwa hamu kwakuwa wamepata nguvu ya pamoja na anagombea kwa msimu mwingine wa nne huku chama chake cha CDU(Christian Democratic Union) kikishika nafasi ya tatu nyuma ya chama cha Demokrasia ya kijamii(SDP) na Alternative fur Deutschland(AfD) kwenye chaguzi za majimbo, waandamaji kumsakama wakitaka aachie ngazi  kwa kuruhusu wahamiaji  mwaka 2015 nchini Ujerumani  tena siku ya kumbukumbu ya miaka 26 ya muungano wa Ujerumani “Germany Unity Day” mapema Oktoba 3, mwaka huu  ila hajapata kigugumizi na vyama vyote vitamsapoti mwakani 2017 kwenye uchaguzi. Kutilia mkazo hasa ndani ya EU (Umoja wa Ulaya) kuwa na sauti  ya mamuzi kutosikiliza sauti ya nchi moja kutokana na ukubwa. Moja kwa moja  mfano ni Uingereza, “mzizi” wa yeye mpka kuja kujitoa EU. “Aliona haiwezekani nchi ndogo kama Ugiriki anaisaidia bajeti yake halafu wawe na maamuzi sawa” nawaza hivyo,  Ukifuatilia kwa undani wanahusika pia kinamama.
Mahakama ya kiuhalifu ya kimataifa (ICC) ina mwanamama Mgambia,  mwendesha mashtaka mkuu(The Hague), anaitwa Fatou Bensounda ni mkakamavu mwenye maamuzi ya kijasiri asingewekwa pale,  kuna kitu cha ziada anacho kuanzia alipoiongoza wizara ya Sheria Gambia kabla ya kuteuliwa mwaka 2012.
Mwendesha Mashtaka ICC, Mama Fatou Bensounda.
Umoja wa Mataifa(UN)  daah! “wamechana mkeka” kwa mwanamama kurithi nafasi ya Ban Ki-Moon, mreno Antonio Gueterrez  kachukua, japo changamoto aliiona  ukiangalia nafasi ya wagombea 12, nane  walikuwa ni wanawake wa shoka  na “nilibet” kinamama watang’ara kama Christiana Figueres, Irina Bokova,  au Hellen Clark na baadhi yao wapo kwenye “ukubwa” wa mashirika ndani ya UN, bado tutaona “impact” yao.
Unajua ubongo wangu unawaza nini? kwenye  zama zakwenye  “fifty-fifty” haya maswala ya kutafuta usawa na haki kwenye mfumo dume ndiyo sauti hizi nyororo utapokwenda kufurahia hotuba na maamuzi zao! Ndio utazifurahia, Taratibu utanielewa!
Harakati za kuzuzururisha akili mataifani  kwa tafakuri na Wabasi wangu, tunaoamini kwenye falsafa za Ubasi, Amani akadai “Msuguano hatarishi wenye harufu ya chechendani ya miaka kumi inaweza tokea kupitia hili kwani kina Putin na wenzake kupinga sera za kihafidhina watazidi kubisha ila hisia zitawapanda kwa wao kuona sauti nyororo zinawapelekesha”, kati ya wale nane  mmoja angechukua, “anyway”  UN wamechana mkeka!
“Pia sauti nyororo zitaona zinapingwa sana nazo zitaingiza hisia kuonyesha  dunia maamuzi yao yalivyo ili heshima ionekane”.
 “Eti msuguano hatarishi ndio  utatokea? Hasa kwenye miaka kumi, wakati wengi wa hawa viongozi watatawala kwa vipindi visivyozidi vinne?” Akajibu mbasi mwingine kwa jina la Mlang’a.
Wakati tafakuri ikiendelea  mara kuna bajaj ikapita na bonge la mziki “me and you na, perfect combo, eeh na perfect combo….”
“Perfect Combo”, ndio ameimba mwanarapu Joh Makini wimbo aliomshirikisha Mnigeria Chidinma, nikawaambia wabasi wangu kuwa kweli hii itakuwa “Perfect Combo”  kwakuwa maamuzi, misimamo, dukuduku, matarajio yao yanaelekea kwenye mrengo mmoja wa kusaidia kizazi cha kinadada kwa kuwatia nguvu ya kujiamini kutoyumbishwa na misimamo ya mfumo dume iliyokwepo, na hata ukisikiliza kwa umakini hotuba zao wanavyojielezea na hasa usawa wa kijinsia na haki unavyojielekeza kuna mabadiliko watafanya, tena makubwa ya kimapinduzi.
Ni suala sio la kipuuzi au kupepesa macho kuukataa ukweli, bado wanaume na hata baadhi ya wanawake tunaamini  nguvu ya hoja kuhusu mfumo dume, waaminio biblia wanaamini mstari usemayo “……..kweli itakuweka huru”, wengi wanatetea kwenye umma kinafiki wakikutana sirini mfumo dume ndio hoja,  Twende taratibu, nadhani unaanza kunielewa!
Kinamama hawa wanaunganisha “nguvu” ya pamoja ukizingatia nchi na taasisi wanazotoka nazo zina “nguvu” za kuitawala dunia kwa masharti yao itakavyo, wana mamlaka kubwa, wataalamu wa kutosha, na uchumi mkubwa ambao ndio “silaha” ya kuteka dunia ya tatu, japo sio nchi zote zinaweza kutingishwa!
Kweli sio nchi zote zinaweza kutingishwa? Hapa ndipo kwenye ule msuguano hatarishi utakao leta cheche mbasi wangu aliounena, na nisiuopenda kuuona ila, unaweza kutokea.
 Je, misimamo ya  mataifa na taasisi zao kwenye kutoa maamuzi na kuingilia mataifa inapingwa na imeathiri vipi dunia hasa mataifa yasiyo na udini na huu unaoitwa ubeberu? Hapa namuwaza sosholisti Vladimir Putin wa Urusi, Kim  Jong-un wa Korea Kaskazini  na Xi Jinping wa China. Kwanini msuguano utakuwa mkubwa sana na kupelekea msuguano hatarishi wenye cheche?
Sauti nyororo kutoa “speech” nzito kutoakana na mataifa na taasisi nzito, na ndipo napata kigugumizi kwa kuwaona wapingaji hawa kutoka mataifa haya yanayokataa kwa uwazi ubeberu nawazungumzia  Korea Kaskazini,  China, Cuba na Urusi. Mnanielewa sio?
Je, Waarabu hasa Mashariki ya kati na misimamo yao ya kidini na utamaduni wao, kwenye hii ‘fifty-fifty”  na “order” ya sauti nyororo  wataelewa, kwakuwa tu, kule kwao hata gari kinamama hawaruhusiwi kuendesha!
Na nguvu ya utekelezaji wa sera zao wanaweza kuzipenyeza kwa namna yoyote ile hata kwa nguvu, angalia Uganda kusitishiwa misaada kisa kupinga sheria za ndoa ya jinsia moja, misaada wamekata!
Sio hatuwezi kusimama bila wao, ila mifumo ilishazoea hiyo hali hivyo lazima mkatae huku haijasitishwa, hapo sitaki kupagusia kwakuwa sio “engo” husika. Akili haipo sawa“ UN wamechana mkeka”. Sio “kesi”, kwanini?
Maamuzi ya dunia yanategemea sana haya mataifa na taasisi hizi, kumbuka suala la demokrasia na mfumo wa vyama vingi  kwenye dunia ya tatu uliletwa na shirika la fedha duniani (IMF) kupitia mpango waliouita “Structural Adjustment Programme”, zaidi  Marekani ndiye mama wa sauti za kutaka mambo yaende atakavyo, siasa ya dunia kaikalia na anaijua, nchi na taasisi  zenye nguvu kimaamuzi na utekelezaji duniani zina watu hawa, kwenye nafasi ya wanawake wenye nguvu duniani sita bora Miss Lagarde, Angel Merkel na Hillary Clinton wamo.
Sasa sidhani kama hawa wapingaji wa sera za mabeberu, watarudisha kuni nyuma kutochochea moto, upande wa pili ukiweka mkaa!  Mnanielewa sio?
Sio  kitu cha kushangaza kwenye mifumo yenye mizizi ya kidini, kikabila, kijamii na mazoea vilikuwa vinapinga na havioni nafasi ya mwanamke kwenye mambo makubwa, jiulize ile presha ya kupinga itaongezeka au kupungua kwa asilimia ngapi? 
Sitamani kuzidi  kuziona ghiliba za nchi wanachama wa ubeberu zilivyo na ushirikiano toka muda mrefu. Tangu enzi za vita ya pili ya dunia, Marekani na Uingereza huku taasisi ya IMF na UN zote zipo Marekani na zaidi yule mwanamama kiongozi wa IMF ni mfaransa, sapoti kubwa inaongezeka!
Mnanielewa sasa? maslahi na maamuzi nguvu ya kura “veto” ndani ya UN, na hasa ndani ya baraza la usalama ambapo China na Urusi wapo ila Marekani, Uingereza na Ufaransa  nao ni memba  wa kudumu na jinsi nchi  hizi zilivyo na ukaribu watazidi kulekeza nguvu kwenye maslahi yao kidunia na upande wa pili ni dhahiri hawatokaa kimya.
Ninapoangalia nguvu ya sauti nyororo ipenyayo masikioni bila kutumia nguvu, ila maneno yapenyanyo yanaweza kuwa na zuri au baya, ukicheza tu huponyoki. Ila masoshalisti na wenye “imani kali” watapindua unyororo wa sauti hiyo, na sauti hizi“zitajiongeza” kwa kutumia hisia, nini kitatokea? Msuguano hatarishi!
Bado natafakari baada ya miaka nane mpaka kumi ya vipindi vya sauti hizi nyororo karibu zote zikiachia ngazi. Dunia itaingia kwenye hatua kuelekea historia, kwa wale  “Standpoints feminists” wanayoiamini, japo UN wametuchania mkeka mimi na Wabasi wangu  katika fikra pana, mwanafalsafa E.Maqway na  ndugu Amani.
“End will justifies the meaning” Waingereza husema!