Saturday 15 October 2016

HISTORIA ILIOJEE: DEO FILIKUNJOMBE



Ni  historia iliojee tayari kwa aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Ludewa,  moja kati ya miiba iliyokuwa inachoma Serikali katika mijadala ya Bunge  japo ni mwanaCCM mwenzao, siku kama ya leo  ni kumbukumbu ya kifo chake alifariki dunia kwenye ajali ya helicopter iliyoanguka kwenye eneo la msitu wa mbuga ya Selous. Si mwingine ni ndugu Deogratius Filikunjombe “Deo”  mzaliwa wa wilaya ya  Njombe(sasa mkoa wa Njombe)  Machi 4, 1972.
Ndugu Deogratius Filikunjombe akiwa na abiria wengine wawili pamoja na rubani Kapteni William  Silaa, walikutwa wamekufa katika eneo la ajali  Oktoba 16, 2015.
Polisi walithibitisha kutokea kwa ajali hiyo ya Chopa, chapa 5Y-DKK, iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kuelekea Ludewa. Taarifa za awali zilitolewa na  mgombea ubunge jimbo la Ukonga kupitia CCM siku hiyo, Mh. Jerry Silaa, aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram sbaada ya tukio, alifafanua kuwa baba yake Kapteni  Silaa ndiye alikuwa rubani na kwamba mawasiliano kutoka eneo la tukio, yalikuwa magumu licha ya juhudi kubwa zilizokuwa zikifanywa na vyombo husika kutafuta eneo la ajali.



Ndugu Filikunjombe, akifahamika kama Deo Haule  aliitumikia taaluma yake ya mawasiliano ya umma  akiwa Kampala, Uganda akiripotia kituo cha ITV/Radio One..
Ameondoka lakini atakumbukwa kwenye bunge la kumi kwa kuchachafya vilivyo, pasipo kuwa na uchama kwenye mambo ya kitaifa, hasa alipokuwa akizungumzia “issue” ya ESCROW. Kwa vijana wa kileo alibeba karisma ya “kutotekwa” na uchama kwenye kutetea maslahi ya wananchi kama viongozi wengine, hivyo anatujenga kwa “ombwe” la kimaslahi ya kivyama “lisituoe”  Kitaalamu alikuwa ni msomi wa shahada ya Mawasiliano ya Umma aliyotunukiwa Chuo Kikuu cha Makerere nchini, Uganda.  Alijiunga na Jeshi la Polisi na kufanya kazi kwa mwaka mmoja kisha akaacha kazi , baadaye  alipangiwa kitengo cha Habari makao makuu ya Polisi na kufanya kazi kwa mwaka mmoja. Bada ya Polisi alijiunga na World Vision kama  Afisa Mawasiliano(Communication/Information Officer)  na kufanya kazi kwa miaka kama minne hivi akiwa Makao makuu Arusha na baadae akahamishiwa tawi la Dar es salaam.
Alipotoka World Vision akajiunga na MKURABITA,  ambapo alifanya kazi kwa muda usiozidi miaka miwili akaacha.
Baada ya kuacha MKURABITA, akafungua duka lake la “electronics” lipo Benjamin Mkapa Tower, opposite na Posta Mpya ghorofa ya kwanza. Baadaye akaafungua vituo vyake vya kuuzia mafuta Ludewa na ndipo akaanza harakati za kuingia kwenye siasa na kuchaguliwa kuwa mbunge mwaka 2010. Inasemekana alikuwa hapendelei  kuwa mwanasiasa, japo baba yake alikuwa mkongwe wa TANU.
Mpaka anafariki ameacha mke na watoto wa tatu wa kiume.
Deo (kushoto) akiwa na mmoja wa rafiki zake  Bw. Zitto Kabwe enzi za uhai wake


Kwa vijana wa kileo alibeba karisma ya “kutotekwa” na uchama kwenye kutetea maslahi ya wananchi kama viongozi wengine, hivyo anatujenga kwa “ombwe” la kimaslahi ya kivyama “lisituoe”  bali siku kama ya leo ndiyo alitutoka!
Kwa sisi WAUNGWANA ni HISTORIA ILIOJEE tutamkumbuka!


No comments:

Post a Comment