Ni historia iliojee tayari kwa aliyekuwa mgombea
ubunge jimbo la Ludewa, moja kati ya
miiba iliyokuwa inachoma Serikali katika mijadala ya Bunge japo ni mwanaCCM mwenzao, siku kama ya
leo ni kumbukumbu ya kifo chake alifariki
dunia kwenye ajali ya helicopter iliyoanguka kwenye eneo la msitu wa mbuga ya
Selous. Si mwingine ni ndugu Deogratius Filikunjombe “Deo” mzaliwa wa wilaya ya Njombe(sasa mkoa wa Njombe) Machi 4, 1972.
Ndugu Deogratius Filikunjombe akiwa na abiria
wengine wawili pamoja na rubani Kapteni William Silaa, walikutwa wamekufa katika eneo la ajali
Oktoba 16, 2015.
Polisi walithibitisha kutokea kwa ajali hiyo ya Chopa, chapa 5Y-DKK, iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kuelekea Ludewa. Taarifa za awali zilitolewa na mgombea ubunge jimbo la Ukonga kupitia CCM siku hiyo, Mh. Jerry Silaa, aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram sbaada ya tukio, alifafanua kuwa baba yake Kapteni Silaa ndiye alikuwa rubani na kwamba mawasiliano kutoka eneo la tukio, yalikuwa magumu licha ya juhudi kubwa zilizokuwa zikifanywa na vyombo husika kutafuta eneo la ajali.
Polisi walithibitisha kutokea kwa ajali hiyo ya Chopa, chapa 5Y-DKK, iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kuelekea Ludewa. Taarifa za awali zilitolewa na mgombea ubunge jimbo la Ukonga kupitia CCM siku hiyo, Mh. Jerry Silaa, aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram sbaada ya tukio, alifafanua kuwa baba yake Kapteni Silaa ndiye alikuwa rubani na kwamba mawasiliano kutoka eneo la tukio, yalikuwa magumu licha ya juhudi kubwa zilizokuwa zikifanywa na vyombo husika kutafuta eneo la ajali.
Ndugu
Filikunjombe, akifahamika kama Deo Haule aliitumikia taaluma yake ya mawasiliano ya
umma akiwa Kampala, Uganda akiripotia
kituo cha ITV/Radio One..
Ameondoka
lakini atakumbukwa kwenye bunge la kumi kwa kuchachafya vilivyo, pasipo kuwa na
uchama kwenye mambo ya kitaifa, hasa alipokuwa akizungumzia “issue” ya ESCROW. Kwa vijana wa kileo alibeba karisma ya
“kutotekwa” na uchama kwenye kutetea maslahi ya wananchi kama viongozi wengine,
hivyo anatujenga kwa “ombwe” la kimaslahi ya kivyama “lisituoe” Kitaalamu alikuwa ni msomi wa shahada ya
Mawasiliano ya Umma aliyotunukiwa Chuo Kikuu cha Makerere nchini, Uganda. Alijiunga na Jeshi la Polisi na kufanya kazi kwa mwaka
mmoja kisha akaacha kazi , baadaye alipangiwa kitengo cha Habari makao makuu ya
Polisi na kufanya kazi kwa mwaka mmoja. Bada
ya Polisi alijiunga na World Vision kama Afisa Mawasiliano(Communication/Information
Officer) na kufanya kazi kwa miaka kama
minne hivi akiwa Makao makuu Arusha na baadae akahamishiwa tawi la Dar es salaam.
Alipotoka World Vision akajiunga na MKURABITA, ambapo alifanya kazi kwa muda usiozidi miaka miwili akaacha.
Baada ya kuacha MKURABITA, akafungua duka lake la “electronics” lipo Benjamin Mkapa Tower, opposite na Posta Mpya ghorofa ya kwanza. Baadaye akaafungua vituo vyake vya kuuzia mafuta Ludewa na ndipo akaanza harakati za kuingia kwenye siasa na kuchaguliwa kuwa mbunge mwaka 2010. Inasemekana alikuwa hapendelei kuwa mwanasiasa, japo baba yake alikuwa mkongwe wa TANU.
Alipotoka World Vision akajiunga na MKURABITA, ambapo alifanya kazi kwa muda usiozidi miaka miwili akaacha.
Baada ya kuacha MKURABITA, akafungua duka lake la “electronics” lipo Benjamin Mkapa Tower, opposite na Posta Mpya ghorofa ya kwanza. Baadaye akaafungua vituo vyake vya kuuzia mafuta Ludewa na ndipo akaanza harakati za kuingia kwenye siasa na kuchaguliwa kuwa mbunge mwaka 2010. Inasemekana alikuwa hapendelei kuwa mwanasiasa, japo baba yake alikuwa mkongwe wa TANU.
Mpaka anafariki ameacha
mke na watoto wa tatu wa kiume.
Deo (kushoto) akiwa na mmoja wa rafiki zake Bw. Zitto Kabwe enzi za uhai wake |
Kwa vijana wa kileo
alibeba karisma ya “kutotekwa” na uchama kwenye kutetea maslahi ya wananchi
kama viongozi wengine, hivyo anatujenga kwa “ombwe” la kimaslahi ya kivyama “lisituoe” bali siku kama ya leo ndiyo alitutoka!
Kwa sisi WAUNGWANA ni
HISTORIA ILIOJEE tutamkumbuka!
No comments:
Post a Comment