Kinda Rasheed Al Hajjawi |
Mabingwa
hao wa Italia, Juventus wamemchukua “kinda” mpalestina Rasheed Al Hajjawi mwenye miaka 10,
baada ya kuzungumzwa sana kwenye “media: za kiarabu siku za karibuni. Licha ya
kukulia mjini Gaza, “kinda” huyo alizaliwa na kukulia Norway.
Habari za kunaswa kwa
kinda huyo zimekuja baada ya “skauti ya kisasa” ya kunyaka matukio, habari na
vipaji ya mtandao wa kijamii kupitia Youtube, huku wakibashiri kuwa ni Lionel Messi mpya. ndani ya wiki ya karibuni siku ya Jumanne pia kumetokea dogo mwingine kwa jina la Karamoko Dembele mwenye miaka 13, aliyefanya "appearance" kwa
dakika 10 za mwisho kwenye mechi ya Celtic U20's katika ushindi wa goli 3-1
dhidi ya Hearts.
Dembele akiingia uwanjani |
DOGO SI WA MCHEZOMCHEZO
Kweli si wa
mchezomchezo kabla ya kutua alishaibuka kwenye mazoezi ya klabu ya Liverpool,
na pia kuwa karibu na mastaa wa Real Madrid.
Dogo Rasheed akiwa Liverpool |
Kwenye mtandao wa “facebook” dogo kazitundika picha za mastaa kadhaa
aliopiga nao stori.
No comments:
Post a Comment