Tuesday 11 October 2016

HAPPY EARTHSRONG "SHUJAA" SIR BOB CHARLTON

Sir Bob Charlton enzi zake.
Leo bwana ndiyo “birthday”  ya shujaa Sir Robert "Bobby" Charlton alizaliwa  11 Oktoba  1937. Ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu wa Uingereza, Anajulikana kama mmojawapo wa viungo wa kati wenye uwezo wa hali ya juu wa muda wote. Nembo muhimu katika timu ya taifa ya Uingereza ambapo alishinda Kombe la Dunia na Ballon d'O r mwaka 1966. Yeye alicheza karibu muda wote katika klabu yake  ya Manchester United, ambapo alikuwa mashuhuri kwa uwezo wake wa kushambulia na kupiga mashuti yaliypachikwa jina "Long Lange Shot" yaliyopigwa toka umbali mrefu. Alionywa kwa kadi mara mbili tu katika maisha yake ya soka; mara moja dhidi ya Argentina mwaka 1966 katika Kombe la Dunia, na katika mechi ya ligi kuu dhidi ya Chelsea. Alizaliwa huko Ashington, Northumberland. Charlton alicheza mechi yake ya kwanza kwa Manchester United katika kikosi cha kwanza mwaka 1956, na zaidi ya misimu miwili alipata nafasi ya uhakika katika timu. Ni moja ya wachezaji walionusurika katika ajali ya anga mjini Munich mwaka 1958 baada ya kuokolewa na Harry Gregg, baada ya kuisaidia timu ya Mashetani Wekundu kushinda kombe la Football League mwaka 1965 pia alishinda Kombe la Dunia na medali katika timu ya taifa ya Uingereza mwaka 1966 na kombe la “Football League” akiwa na Mashetani Wekundu mwaka uliofuata. Mwaka 1968 akiwa nahodha wa Manchester United alishinda Kombe la Ulaya akifunga mabao mawili katika mechi ya fainali . Amefunga mabao zaidi kwa United (249) kuliko mchezaji mwingine yeyote na kutokea kuwa mfungaji bora England wa muda wote  wa timu ya Taifa kwa mabao 49  na Wayne  Rooney kumpiku juzi kati kwa goli 50 katika mechi 107 alizocheza.


Hivyo kuanzia Mei 1968 hadi Septemba 2015, kwa Rooney kuvunja rekodi hiyo ndani ya Uingereza. Bobby Charlton alikuwa na rekodi ya kucheza mechi nyingi kwa Manchester United (758), kabla ya kuzidiwa na Ryan Giggs. Aliichezea Uingereza mara nne katika Kombe la Dunia (1958, 1962, 1966, na 1970), na kuisaidia Uingereza kushinda shindano hilo mwaka 1966.
Sir Bob Charlton siku za karibuni
Wakati wa kustaafu kwake kutoka timu ya England mwaka 1970, alikuwa ameichezea timu ya Taifa mechi nyingi kuliko mchezaji yeyote (mara 106 katika ngazi ya juu) ila Wayne Rooney kaivunja kwa mechi 107, kwa aliyocheza  mwaka jana dhidi ya Uswisi. Rekodi hii tangu wakati huo ilikuwa kwa upande wa Bobby Moore na Peter Shilton. Aliondoka Manchester United na kuwa meneja wa Preston North End katika msimu wa 1973-1974. Ambapo alikuwa mchezaji-meneja na baadaye kuwa mkurugenzi wa Wigan Athletic, Msimu uliofuata akawa mwanachama wa bodi ya wakurugenzi Manchester United tangu mwaka 1984 mpaka sasa msimu wa 2016/17.


Huyu ndiye Sir Robert "Bobby" Charlton aliyeshikilia rekodi ya ufungaji wa mabao Uingereza kwa miaka 47, HAPPY BIRTHDAY LEGEND!



Unakaribishwa kuacha comment yako hapo chini!

No comments:

Post a Comment