Mchezo wa VPL kati ya Simba iliyokuwa
mwenyeji wa Kagera Sugar umemalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa goli mbili
kwa bila.
Magoli ya Simba yamefungwa na beki
Mzarimu Yassin akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Shiza Kichuya katika
dakika ya 44 na goli la pili likifungwa na Shiza Kichuya kwa mkwaju wa penati
katika dakika ya 75.
Ushindi huo unaiwezesha Simba kufikisha
alama 23 katika michezo tisa iliyocheza, ikishinda michezo saba na kutoa sare
miwili na ikiwa na mchezo mmoja mkononi, Kagera Sugar inasalia kuwa na alama 15
ikiwa katika nafasi ya tatu ya msimamo wa VPL.
No comments:
Post a Comment