Naibu Waziri wa Elimu, Injiania Ester Mayanja |
Akizungumza na
waandishi wa habari Naibu Waziri Elimu,Sayansi na Teknolojia, Mhandisi Stella
Manyanya alisema, “Tumeangalia sifa zifuatazo: fani ya kwanza tumesema awe
kwenye fani ya sayansi za tiba na afya, ya pili ualimu wa sayansi na hisabati,
ya tatu uhandisi wa viwanda,kilimo, mifugo, mafuta na gesi asilia, sayansi
asilia na sayansi ya ardhi,ufanisi majengo na miundo mbinu.”
“Lakini pia
tumesisitiza wale wenye mahitaji maalum,kama vile ulemavu na uyatima,lakini
hata tukisema kwamba uyatima hatumaanishi yatima mwenye uwezo, maana yake
anaweza kuwa amefiwa na mzazi mmoja mwingine yupo lakini pia mzazi
aliyetangulia ameacha fursa za kutosha kiasi kwamba hali ni nzuri,huyo tunasema
yule ambaye ni yatima maskini,”alisisitiza.
“Vile vile ufaulu, na
ufaulu huo uwe katika maeneo yale ya vipaumbele kwa mfano unaweza ukawa
umefaulu masomo ya kukuwezesha kuingia kwenye sayansi pengine ufaulu wako hauko
wa juu sana, pengine tuchukulie tutaanza na wa division 1, wakishajaa unaingia
2, wakishajaa unaendelea. Kwahiyo hatutaweza kumchukua wa chini wakati mwingine
wa juu bado hajapata kwasababu hiyo inatusaidia katika upimaji wa
haki,”aliongeza.
Aidha mhandisi
Manyanya amesema kuanzia mwaka huu wa masomo wanufaika wote wa mikopo
watakopeshwa kulingana na uwezo wao kiuchumi katika vipengele vyote vya mikopo.
Hii hapa “press release” ya taarifa hiyo;
No comments:
Post a Comment