Rapper Coolio |
Waendesha mashtaka
nchini Marekani wanasema kuwa bunduki hiyo aina ya handgun ilipatikana katika
mzigo wake wakati wa ukaguzi katika uwanja wa ndege wa LAX mwezi uliopita.
Coolio mwenye umri wa
miaka 53 huenda akahukumiwa kifungo cha hadi miaka 3 katika jela ya jimbo la
Carlifornia iwapo atapatikana na hatia.
Coolio ni maarufu kwa
wimbo wake Gansta Paradise ambao ulitolewa mwaka 1995. Ameshtakiwa chini ya
jina lake Artis Leon Ivey.
Waendesha mashtaka wanasema ilikuwa kinyume cha sheria
kwa msanii huyo kubeba bunduki baada ya kupatikana na hatia mwaka 2001 kwa
kubeba bunduki ndani ya gari na mwaka 2009 kwa kumiliki dawa ya kulevya aina ya
Cocaine.
Nyota huyo alitarajiwa kuwasili
katika mahakama ya Los Angeles siku ya Alhamisi lakini kusikizwa kwa kesi yake
kukaahirishwa hadi Oktoba 26.
Mawakili wa Coolio walimwambia
Jaji kwamba msanii huyo alikuwa anawatumbuiza mashabiki wke nje ya jimbo la
California na hivyobasi hawezi kuwa katika mahakama hiyo.
No comments:
Post a Comment