Friday 14 October 2016

“Argue, Don't Shout" Ya Mwalimu Nyerere Tuiishi Kwa Vitendo

Hii ni makala niliyokuwekea uisome hapa Oktoba 14, ila siku iliyofuata Oktoba 15, 2016  imepata nafasi kwenye gazeti la TanzaniaDaima
   
   
Na 
Peter C. Mmbaga

Ndiyo muda wangu wa kuingia “Giningi” na Wabasi  wenzangu ambao tunaamini kwenye mawazo ya  chanya pasipo kupepesa  macho, safari ya Giningi inahitaji ufunge mkanda kweli kweli na leo nipo njiani kuongea na  kumpa pongezi za  “kuondoka” zake mapema mbasi wangu katika fikra Mwalimu mkuu, Baba Makongoro  kwakuwa angebaki mpaka sasa angekuwa anaduwaa kama mimi na vile hapendi  kuonekana  kwenye   “maamuzi  ya umimi”,  anakuwa mpole tu.
Kumbuka kipindi kile wakisema  baadhi ya viongozi   waliokuwa wanafanya mambo  tofauti, yeye alitoa tamko gani? Kwenye kitabu chake cha “Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania” anabaki kama mshauri tu, japo kutokana na hadhi yake ama “popularity” aliyokuwa nao asingesikilizwa na wananchi kweli, katika kukataza?
Aliwaachia uhuru wajitathimini  wenyewe, na uhuru ni mbaya sana, walipoona   mbasi wangu katika fikra  chanya hajaja juu wakaona sawa tu, mambo yanafanyika,  anajifanya haoni. Kumbe “mbasi” ulikuwa “unawachora” tu.
“Giningi yetu” ina raha yake huku yupo Baba wa maridhiano, mbasi wangu katika fikra, Mandela yeye anatabasamu tu anasema “Real leaders must be ready to sacrifice  all for the freedom of their people“ kwa tafsiri isiyo rasmi ni kuwa “ Vingozi wa kweli wanatakiwa wawe tayari kujitoa vilivyo kwa  uhuru wa wananchi”, naye namwangalia natabasamu  kwa kuwa kazi aliyoiamua  Rais JPM ni ngumu  sana kwakuwa  wapiga vita mfumo  mzuri wapo  na hasa watendaji, “We got a Long Way To Freedom” ila kwa imani atawatumbua tu!
Baba Makongoro bwana ananifurahisha sana akasema “Siku Wamarekani wakinisifia nimefanya kazi nzuri nitajiuliza kuwa nimekosea wapi?”  ndiyo kitu nilichompendea hasa kwa kauli hizi za kujiamini kwa nukuu nilyooina kwenye gazeti moja la kila siku miaka mitatu nyuma, ni kauli ya Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), chuo ambacho Mwalimu alikianzisha na mara kwa mara kufika hapo kwa ajili ya mijadala na wanafunzi kuhusu uhuru na maendeleo ya Afrika na dunia kwa ujumla, Bashiru Ally, anaamini Mwalimu anastahili  kupewa tuzo  lakini ananyimwa kutokana na kuyaudhi mataifa ya magharibi wakati aliongoza harakati za kudai haki za binadamu na uhuru wa mataifa ya Afrika. Huu ndiyo ushujaa tunaouhitaji Rais JPM piga kazi kwa haki na kweli usihitaji kusifiwa na watu wa nje ila tu angalia uhuru uwepo kama Baba Makongoro alivyoutoa. Mwalimu vijana wa leo sio wa kipindi kile  “pesa” inawanunua wanashindwa kutetea maslahi ya nchi,  hasa wasomi dira hawaileti , ukanijibu “pesa ni matokeo” kama ulivyoainisha kwenye kitabu chako cha cha “Ujamaaa na Kujitegemea” lakini Mwalimu sasa sivyo, nadhani wakati nao unabadilika, ila  wanaamini,  pesa ndilo lenye nguvu!
Sasa hivi wasomi wanaonekana shujaa  kwenye dimbwi la mfumo  huu wakuogopa kuhoji, vyuo vikuu vimepoa  vimenyamaza, nahisi huko ndiko ulipowasikia kwa mara ya kwanza   kina ndugu Lowassa, JK  na wengineo,   ila sasa wanaogopa  kuitwa wasaliti ni bora kuliko kuonekana mnyenyekevu kwao halafu kwenye jamii uonekane “Kamuzu”. Wazee wetu  ukiwauliza watakujibu enzi za kupigania uhuru walimwita   huyu mtu walimwitaje  "aliyeolewa na wazungu" aliwabania waafrika haki zao, ndiyo nyimbo iliyokuwa kwenye mchamchaka.
Kwanini nimesema hayo?  Nakumbusha raia wote  na viongozi wasaliti kwa machinga, boda boda, mama ntilie , wasakatonge , wasio na ajira ni bora uonekane umemsaliti rafiki yako anayetafuta  “ujiko” kwa njia ya  “matukio” kuliko kuitwa "umeolewa nao" na jamii ni mbaya sana,  lakini Mwalimu hao watu tunao?
Wewe mwenyewe ukasema “Unyenyekevu ukizidi unazaa uoga, uoga huzaa unafiki na kujipendekeza, mwisho wake mauti”
Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu J.K Nyerere

Baba Makongoro kuna walimu  wamekuwa  ‘maarufu” kwa kipindi hichi kubwa ni kumpiga mwanafunzi  wa kidato cha tatu mwezi huu uliotuaga, kuna kitu baba nimegundua Walimu wengi wanakwenda pasipo ‘passion”, lengo ni kupata mkopo ambao miaka ya karibuni imekuwa  kipaumbele kwa walimu ili kusaidia changamoto za elimu yetu, japo wanafunzi wa siku hizi ni watukutu kufikia hatua ya kuchanganywa na malezi na utandawazi ambao tumeupokea “negative” sana kwenye matumizi yake.
Mtoto  kupewa adhabu hatujakataa, ni moja ya kufunza baba, kama wewe ulifanya pale Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam kwa mmoja wa viongozi wetu kugoma akiwa  Rais wa serikali ya wanafunzi-Daruso  enzi zako  wakigomea kutopatiwa maziwa na siagi, kweli enzi zako “walikula bata”  mbasi wangu, leo hii wanasota watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu  “no mkopo”, kipaumbele kimeharibu kila kitu na wengi wanakimbilia huo ualimu,  tasnia nyingine baada ya miaka kumi wasomi wengi watakuwa kwenye  tasnia moja halafu wasio na “passion” japo sio wote ama tasnia zote lakini Je, hali itakuwaje?
Enzi zako mtu akisema mimi ni mwalimu hiyo heshima anayopewa  ni nzito lakini leo sielewi, thamani imepungua sijui kisa ni nini? Ndo maana misongo ya mawazo  inakuwa mingi sana hata kupiga wanafunzi.
Mimi kusema kula bata ni kweli kwasababu   habari  hii niliwahi  kuhadithiwa na “anko” wangu aliyesoma na ndugu Rais  mstaafu kijana wako, Jakaya  Kikwete pale Shule ya Tanga (Tanga  School) enzi zako  Mwalimu Mkuu wa fikra yakini,  juu ya elimu,chakula(asubuhi chai nzito), na usafiri wa  bure kwa gharama za Serikali.  Ila nyakati zinabadilika!
Wakati tunaendelea na maongezi yetu ya Kibasi zaidi huko “Ginigi yetu”  kuna  msomi  enzi zake Mwalimu  akaniuliza leo hii madaftari  yanauzwa  kwa shilingi ngapi  wanafunzi, vipi madawati shuleni?  Nikamwambia najua, wajua, akanijibu halafu tuna misitu mikubwa nchini?
 Baba Makongoro ulivyooondoka kuna mwana hip hop aliimba “wasomi wanakimbilia siasa, Je, nchi itajengwa na nani? Hata mimi najiuliza nchi itajengwa na nani? Sielewi!

Mwalimu alizidi  nitoa tongotongo katika kuandaa  na maswala mengine yenye maslahi kitaifa yasiyohitaji mgawanyiko wa itikadi na uchama  kwa kile  waingereza wanachosema “number do not lie” wakimaanisha  nambari haidanganyi kwa kufanya mambo kwa  “ tathmini onyeshi” moja ni moja na nane si saba, kwakumshangaa  Waziri mwenye dhamana ya Afya  kukinzana na  Makamu wa Rais, kuhusu upungufu  wa madawa kwenye bohari ya Taifa!
Nakamwambia Mwalimu neno “siasa” ni mwiba kwa wananchi si neno  zuri kulizungumza  japo Rais JPM anawapa matumaini kuwa utendaji wake kwa kiasi chake kuna tija imeonekana Mwalimu,  kabla hatujaendelea zaidi   nikatafakari kuwa  ujasiri ni pale unapojua "siasa" si tatizo bali tatizo ni picha na taswira iliyojengeka mtu kuwa "mwanasiasa" ndani ya jamii na jibu tunalo kwa utendaji mzuri wa viongozi wetu  ili kugeuza neno "politics is dirty game". Itabadilika tu hii hali, kama enzi zako Ualimu ulivyoheshimika leo hii unaonekana taaluma ya kawaida! Sisi wenyewe hatupendi Mwalimu.
Nikamwona kifkra shujaa wa India, Mahatma Ghandi na falsafa yake kuwa “I love your Christ but not your Christianity” nikimaanisha  serikali na vyama vya siasa  ni sehemu salama na sera zenye weledi lakini  walioko ndani yake ndiyo kuna kila aina ya ubaya,udhalimu, na siasa chafu japo kuna wasafi na wenye kweli daima. Naipenda sera weledi yenye utekelezaji, itikadi ninayo,na “imani” kwa  kiongozi na mwananchi  mwenye misingi fanikishi ya kuileta “Tanzania ninayoitamani”, si kauli za kutofautiana  za  “makaisari” wetu na sio  ushabiki wa chama. Haya yakifanikiwa mbona “siasa nyeupe” itaonekana na tuishi ili kumuenzi Baba wa Taifa na hilo ndilo kusudi lake, siku siku ya leo tutoe  “speech” za kumsifia ila  hizo  sifa zake ninyi kiuhalisia na kiutendaji  mnaziishi kwenye vyombo vya habari.
Watanzania ni wepesi wa kusahau kama  zao la “kuamua” litaleta watu makini, wazalendo,wenye dira elekevu, na misimamo binafsi   tutakuwa tumefikia kiwango kikubwa katika “mchakato” wa kujitambua na kuutambua ukweli na ule mtazamo wa siasa ni mchezo mchafu (politics is the dirty game) tukiishi ya Baba Makongoro na sio kuienzi siku yake bila matendo sio maneno. Hata  Baba Makongoro kwenye “mjadala” wetu hapendi hilo swala.
Alichopenda ni “Argue, Don’t shout” na hichi ndicho serikali inakinzana na vyama vya upinzani sana, kwasababu kila mmoja anatoa kinachojipendelea ila tukumbuke tunajenga moja, Tanzania yetu katika siku hii ya kumuenzi Baba wa Taifa sio kwa makelele na sifa kedekede bila kuishi aliyoyaishi!
Pumzika kwa amani Mkuu, muda mwingine tutatembeleana!

Description: https://ssl.gstatic.com/ui/v1/icons/mail/images/cleardot.gif

1 comment: