Wednesday 12 October 2016

JPM AWATAKA WATUMISHI KUREJESHA POSHO


Rais JPM amewataka Watumishi wa Umma walioalikwa katika kilele cha sherehe za Mwenge ambazo zitafanyika tarehe 14 Oktoba kutohudhuria na warudishe posho za safari walizolipwa. 
Viongozi waliotajwa kutakiwa kufuta safari zao za kwenda Bariadi ni pamoja na wakuu wote wa mikoa, wilaya, wakurugenzi wote wa  mamlaka za serikali za mitaa, mameya, na wenyeviti wote wa Halmashauri  za majiiji, manispaa, miji na wilaya pamoja na watumishi ambao huambatana nao wakiwemo madereva na wasaidizi wao ambao kwa idadi hufikia takribani 1,500.
Kwa kuwa sherehe za kilele cam bio za mwenge wa Uhuru huambatana na maandhimisho ya siku ya kumbukumbuku ya Baba wa Taifa, hayati, Mwalimu J.K  Nyerere aliyefariki miaka 17 iliyopita, agizo hilo limewataka viongozi wote wa mikoa na wilaya kubaki katika maeneo yao ya kazi na kujiwekea utaratibu wa jinsi ya kuienzi siku hiyo.

 Hii hapa ni “Press Release” ya taarifa hiyo.

No comments:

Post a Comment