Rais JPM amewataka Watumishi wa Umma
walioalikwa katika kilele cha sherehe za Mwenge ambazo zitafanyika tarehe 14
Oktoba kutohudhuria na warudishe posho za safari walizolipwa.
Viongozi waliotajwa kutakiwa kufuta
safari zao za kwenda Bariadi ni pamoja na wakuu wote wa mikoa, wilaya,
wakurugenzi wote wa mamlaka za serikali
za mitaa, mameya, na wenyeviti wote wa Halmashauri za majiiji, manispaa, miji na wilaya pamoja na
watumishi ambao huambatana nao wakiwemo madereva na wasaidizi wao ambao kwa
idadi hufikia takribani 1,500.
Kwa kuwa sherehe za kilele cam bio za
mwenge wa Uhuru huambatana na maandhimisho ya siku ya kumbukumbuku ya Baba wa
Taifa, hayati, Mwalimu J.K Nyerere
aliyefariki miaka 17 iliyopita, agizo hilo limewataka viongozi wote wa mikoa na
wilaya kubaki katika maeneo yao ya kazi na kujiwekea utaratibu wa jinsi ya kuienzi
siku hiyo.
Hii hapa ni “Press Release” ya taarifa hiyo.
No comments:
Post a Comment