Bibi Titi Mohamed |
Ni HISTORIA ILIOJEE! mwanamke jasiri, shujaa na mwenye msimamo, moja ya barabara kuu ndani ya jiji la Dar es Salaam, jina lake limo kwa heshima ya mchango wake mkubwa wa kuleta uhuru wa Tanganyika.
Si mwingine ni Bibi Titi Mohamed, mwanamama, aliyekuwa kiongozi mmojawapo katika harakati za kudai uhuru wa
Tanganyika, baadaye aliongoza Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT), chama cha
wanawake katika chama cha Tanganyika African National Union (TANU), na baadaye
akawa waziri wa wanawake na masuala ya kijamii katika serikali ya Mwalimu
Nyerere.
Bi Titi
Mohamed alikuwa mwanamke wa Kiislamu aliyezaliwa jijini Dar es Salaam
mnamo mwaka 1926 na baba mfanyabiashara
na mama mkulima. Alipata elimu ya shule za msingi pekee na alipofikisha umri wa miaka 14 tu aliolewa na mume mzee.
Bi Titi Mohamed alipata nguvu ya kuwa mwanaharakati kupitia kipaji cha kuimba, enzi za ujana
wake alikuwa mwimbaji mzuri wa kwasida na hivyo kuwa kama mwimbaji kiongozi katika ngoma katika
kikundi cha muziki na ngoma ambacho kilimwongozea uzoefu wa kuwa mbele ya
umati.
Nguvu ya kushiriki katika majukumu ya uongozi na
uhusiano ndani ya mitandao wanawake na mapambano ya kitaifa yallianza mwaka
1950, baada ya Vita Kuu ya II ya dunia, Tanganyika ikiwemo nchi nyingine katika harakati za uzalendo zilikuwa
zimeshika kasi. Mwaka 1954, TANU iliundwa chini ya uongozi wa mwalimu na baadaye Rais Julius Nyerere.
Bibi Titi na Mwalimu J.K Nyerere kwenye pozi enzi hizo |
Muda si mrefu
baadaye mwaka 1955, Bibi Titi
alikasimishwa kiti cha UWT, na ndani ya
miezi mitatu ya uteuzi wake, walijiunga wanawake zaidi ya 5,000 kama wanachama
wa TANU, na hivyo kwa mrengo huo wa
wanawake uliianzishwa na jukumu kubwa kwa mapambano ya uhuru na UWT
kufanya kazi kubwa ya kukuza maadili ya
TANU kwa raia. Pia umoja wanawake ukapaza sauti moja katika mapambano dhidi ya
ukoloni.
Bibi Titi
kupitia wanaharakati wanawake walikuwa na uwezo wa kutumia mitandao yao
mbalimbali ya kijamii na kiuchumi kwa kuongeza fedha kwa kiasi kikubwa kwaajili
ya chama cha TANU. Zaidi ya hayo, Bibi
Titi akiwa na kipawa cha usemaji, yeye
mwenyewe, alihamasisha wanawake kupitia makundi ngoma na kusimamia viongozi wao
kuunda nafasi kwa ajili ya kushughulikia wanachama na kuwasaidia, pia makundi hayo yalikuwa wazi kwa wanawake wote
waliotaka kujiunga, na kuishia kuwa mitandao yenye nguvu kisiasa ajili ya kubadilishana taarifa, tangazo la mikutano ya kampeni na maandamano.
Mwishowe mafanikio yaliingia mwaka 1961,
kwa Tanganyika kupata Uhuru.
Bibi Titi Mohamed bahati mbaya kisiasa ilimpata mwaka 1965 wakati alipopoteza kiti
chake cha ubunge. Mwaka 1967, yeye alijiuzulu kutoka uwaziri .
Baadaye alipata masaibu ya kisiasa kwa kiasi kikubwa ilifanya kutoweka katika
maisha ya umma na baadaye mnamo Novemba 5, 2000, Bibi Titi Mohamed pumzi yake ilirejea
ilipotoka katika hospitali ya Net Care
huko Afrika Kusini.
HISTORIA ILIOJEE inajivunia Bibi Titi, mwanamama wa
shoka, malkia wa nguvu atakumbukwa kwa
mengi, heshima yake ipo kwenye kutoa mwanga wa harakati za
wanawake dhidi ya mfumo mibovu kwenye kila nyanja ya maisha, kwetu sisi
WAUNGWANA ni HISTORIA ILIOJEEE!
Unakaribishwa kuacha comment yako hapo chini!
Unakaribishwa kuacha comment yako hapo chini!
No comments:
Post a Comment