Saturday 15 October 2016

MSHINDI WA GRAMMY ASHTAKIWA KWA UMILIKI WA SILAHA

Rapper Coolio
Mshindi wa tuzo ya Grammy katika muziki wa Rap Coolio ameshtakiwa kwa kumiliki bunduki haramu.
Waendesha mashtaka nchini Marekani wanasema kuwa bunduki hiyo aina ya handgun ilipatikana katika mzigo wake wakati wa ukaguzi katika uwanja wa ndege wa LAX mwezi uliopita.
Coolio mwenye umri wa miaka 53 huenda akahukumiwa kifungo cha hadi miaka 3 katika jela ya jimbo la Carlifornia iwapo atapatikana na hatia.
Coolio ni maarufu kwa wimbo wake Gansta Paradise ambao ulitolewa mwaka 1995. Ameshtakiwa chini ya jina lake Artis Leon Ivey.
Waendesha mashtaka wanasema ilikuwa kinyume cha sheria kwa msanii huyo kubeba bunduki baada ya kupatikana na hatia mwaka 2001 kwa kubeba bunduki ndani ya gari na mwaka 2009 kwa kumiliki dawa ya kulevya aina ya Cocaine.
Nyota huyo alitarajiwa kuwasili katika mahakama ya Los Angeles siku ya Alhamisi lakini kusikizwa kwa kesi yake kukaahirishwa hadi Oktoba 26.
Mawakili wa Coolio walimwambia Jaji kwamba msanii huyo alikuwa anawatumbuiza mashabiki wke nje ya jimbo la California na hivyobasi hawezi kuwa katika mahakama hiyo.



UJENZI WA RELI MPYA TANZANIA KUHARAKISHWA

Rais wa Tanzania Dkt. John Magufuli akiagana na Waziri wa Biashara toka China, Bw. Qian Keming baada ya mazungumzo, Ikulu jijini Dar Es Salaam

Mradi wa ujenzi wa reli ya kati nchini Tanzania unatarajiwa kuharakishwa kufuatia mazungumzo kati ya Rais John Magufuli na Naibu Waziri wa Biashara wa China Qian Keming.
Reli hiyo ya kati ni ya kutoka Dar es Salaam, Mwanza, Kigoma na inatarajiwa kuunganisha Tanzania na nchi za Rwanda na Burundi
Wakati wa mazungumzo ikulu Dar es Salaam Rais Magufuli alisema serikali inataka kuona mambo yakifanyika na kutoa matokeo bila kupoteza muda, kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu.
Serikali ya Tanzania imetenga shilingi trilioni moja kwa ajili ya kuanza kwa ujenzi katika bajeti ya sasa.
"Sisi tumeamua kuanza ujenzi na tayari Wakandarasi 32 wamejitokeza kuomba kujenga reli ya kati kuanzia Dar es Salaam hadi Morogoro umbali wa kilomita 200 za mwanzo na tutatumia fedha zetu wenyewe," alisema Dkt Magufuli kwa mujibu wa taarifa kutoka ikulu.
"Kazi hii tunataka ianze mwaka huu wa fedha, kwa sababu upembuzi yakinifu na usanifu umeshafanyika, kwa hiyo na nyie ongezeni kasi ili mradi huu wote ukamilike, nataka uwe umekamilika kabla sijaondoka madarakani."
Dkt Magufuli alisema mradi huo una manufaa makubwa kwa Tanzania na nchi nyingine nane zinazotegemea bandari ya Dar es Salaam na kwamba kukamilika kwake kutatoa mchango mkubwa katika ukuaji wa uchumi wa Tanzania ambayo inataka kuwa nchi ya kipato cha kati ifikapo mwaka 2025.
Kwa mujibu wa taarifa ya ikulu, Bw Qian aliahidi kuwa Serikali ya China itaongeza msukumo katika uharakishaji wa utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa reli hiyo ya kati.
"Mheshimiwa Rais Magufuli nimeielewa dhamira yako na kiu uliyonayo, naona kabisa kwamba dhamira ya kisiasa ipo ya kutosha, tunachotakiwa kukifanya ni kuwasukuma wataalamu wetu waongeze kasi," alisema.
„Na mimi nakuahidi kuwa tulikuwa tunakwenda kwa kasi ya kilometa 100 kwa saa, sasa tutaongeza na kwenda kilometa 200 kwa saa."





Chanzo: BBC Swahili




Unaweza toa comment yako hapo chini!

SIMBA I KILELENI

Mchezo wa VPL kati ya Simba iliyokuwa mwenyeji wa Kagera Sugar umemalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa goli mbili kwa bila.
Magoli ya Simba yamefungwa na beki Mzarimu Yassin akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Shiza Kichuya katika dakika ya 44 na goli la pili likifungwa na Shiza Kichuya kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 75.
Ushindi huo unaiwezesha Simba kufikisha alama 23 katika michezo tisa iliyocheza, ikishinda michezo saba na kutoa sare miwili na ikiwa na mchezo mmoja mkononi, Kagera Sugar inasalia kuwa na alama 15 ikiwa katika nafasi ya tatu ya msimamo wa VPL.


LIST YA WACHEZAJI WANAOWANIA TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA, SAMATTA YUMO!

Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Samatta yu miongoni mwa majina yaliyotangazwa  na shirikisho la soka Afrika CAF  katika list ya wachezaji 30 wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2016.
Mtanzania Mbwana Samatta ambaye ni mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2015 kwa wachezaji wanaocheza Ligi za ndani ya Afrika, safari hii amepata nafasi ya kuwania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa ujumla kwa mara ya kwanza akiichezea klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji.
List  nzima ipo hivi;
List ya majina 25 ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ndani ya Afrika.




VIGEZO VYA KUPATA MKOPO VYAWEKWA WAZI

Naibu Waziri wa Elimu, Injiania Ester Mayanja
Kama umekosa mkopo wa bahati mbaya hivi ni vigezo viulivyokuwa vikizingatiwa zaidi, hayo yamewekwa wazi baada ya Bodi ya mkopo ya wanafunzi wa elimu ya juu hapa nchini  kuwa imetangaza majina ya wanufaika wapya wa mkopo kwa mwaka mpya wa masomo 2016/2017.
Akizungumza na waandishi wa habari Naibu Waziri Elimu,Sayansi na Teknolojia, Mhandisi Stella Manyanya alisema, “Tumeangalia sifa zifuatazo: fani ya kwanza tumesema awe kwenye fani ya sayansi za tiba na afya, ya pili ualimu wa sayansi na hisabati, ya tatu uhandisi wa viwanda,kilimo, mifugo, mafuta na gesi asilia, sayansi asilia na sayansi ya ardhi,ufanisi majengo na miundo mbinu.”
“Lakini pia tumesisitiza wale wenye mahitaji maalum,kama vile ulemavu na uyatima,lakini hata tukisema kwamba uyatima hatumaanishi yatima mwenye uwezo, maana yake anaweza kuwa amefiwa na mzazi mmoja mwingine yupo lakini pia mzazi aliyetangulia ameacha fursa za kutosha kiasi kwamba hali ni nzuri,huyo tunasema yule ambaye ni yatima maskini,”alisisitiza.
“Vile vile ufaulu, na ufaulu huo uwe katika maeneo yale ya vipaumbele kwa mfano unaweza ukawa umefaulu masomo ya kukuwezesha kuingia kwenye sayansi pengine ufaulu wako hauko wa juu sana, pengine tuchukulie tutaanza na wa division 1, wakishajaa unaingia 2, wakishajaa unaendelea. Kwahiyo hatutaweza kumchukua wa chini wakati mwingine wa juu bado hajapata kwasababu hiyo inatusaidia katika upimaji wa haki,”aliongeza.
Aidha mhandisi Manyanya amesema kuanzia mwaka huu wa masomo wanufaika wote wa mikopo watakopeshwa kulingana na uwezo wao kiuchumi katika vipengele vyote vya mikopo.
Hii hapa “press release” ya taarifa hiyo;

TCRA YAWATAKA MAWAKALA WASIINGIZE BIDHAA ZA SAMSUNG NOTE 7

Mamlaka ya wawasiliano Tanzania (TCRA) imewataka wafanyabiashara wenye leseni za kuingiza simu nchini, zinazotolewa na mamlaka hiyo, kutekeleza maagizo yaliyotolewa na Kampuni ya Samsung ya kurejesha simu za kisasa za Samsung Galaxy Note 7 baada ya kubainika zina matatizo ya betri. Akizungumza Dar es Salaam Ijumaa hii na gazeti la habari leo, meneja mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy, alisema ni vyema mawakala hao wakatekeleza maagizo hayo, kwani simu hizo ni hatari kuendelea kutumika.

“Simu hiyo tayari Samsung wenyewe wamesema ina matatizo ya betri na mara mbili sasa imelipuka, hakuna faida ya mtu kuendelea kuitumia unaweza ukasababisha hatari kubwa, inapolipuka inaweza kukuondoa mikono, inaweza kulipua nyumba na matatizo mengine tunawataka wenye simu hizo kuziridisha haraka,” alisema Mungy.
“Taarifa tulizonazo haijaingia sana hapa nchini lakini wapo walioletewa kama zawadi kutoka nje ya nchi nawaomba warudishe huko kuepuka matatizo yanayoweza kujitokeza,” aliongeza.
Samsung iliwataka watu waliokuwa wamenunua jumla ya simu milioni 2.5 mwezi Septemba mwaka huu, kuzirejesha madukani baada ya wateja wengi kulalamika kwamba betri za simu hizo zilikuwa zinalipuka. Katika hatua nyingine, wiki iliyopita, Kampuni hiyo ya Samsung ya Korea Kusini ilitangaza kuwa imesitisha utengenezaji wa simu aina ya Galaxy Note 7.

Aidha Mungy aliwataka wananchi ambao tayari wanatumia simu hizo kuzizima na kuzirudisha haraka katika maduka walikozinunua ili kuepusha hatari ambayo tayari Samsung wameshaitoa.


HISTORIA ILIOJEE: DEO FILIKUNJOMBE



Ni  historia iliojee tayari kwa aliyekuwa mgombea ubunge jimbo la Ludewa,  moja kati ya miiba iliyokuwa inachoma Serikali katika mijadala ya Bunge  japo ni mwanaCCM mwenzao, siku kama ya leo  ni kumbukumbu ya kifo chake alifariki dunia kwenye ajali ya helicopter iliyoanguka kwenye eneo la msitu wa mbuga ya Selous. Si mwingine ni ndugu Deogratius Filikunjombe “Deo”  mzaliwa wa wilaya ya  Njombe(sasa mkoa wa Njombe)  Machi 4, 1972.
Ndugu Deogratius Filikunjombe akiwa na abiria wengine wawili pamoja na rubani Kapteni William  Silaa, walikutwa wamekufa katika eneo la ajali  Oktoba 16, 2015.
Polisi walithibitisha kutokea kwa ajali hiyo ya Chopa, chapa 5Y-DKK, iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam kuelekea Ludewa. Taarifa za awali zilitolewa na  mgombea ubunge jimbo la Ukonga kupitia CCM siku hiyo, Mh. Jerry Silaa, aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram sbaada ya tukio, alifafanua kuwa baba yake Kapteni  Silaa ndiye alikuwa rubani na kwamba mawasiliano kutoka eneo la tukio, yalikuwa magumu licha ya juhudi kubwa zilizokuwa zikifanywa na vyombo husika kutafuta eneo la ajali.



Ndugu Filikunjombe, akifahamika kama Deo Haule  aliitumikia taaluma yake ya mawasiliano ya umma  akiwa Kampala, Uganda akiripotia kituo cha ITV/Radio One..
Ameondoka lakini atakumbukwa kwenye bunge la kumi kwa kuchachafya vilivyo, pasipo kuwa na uchama kwenye mambo ya kitaifa, hasa alipokuwa akizungumzia “issue” ya ESCROW. Kwa vijana wa kileo alibeba karisma ya “kutotekwa” na uchama kwenye kutetea maslahi ya wananchi kama viongozi wengine, hivyo anatujenga kwa “ombwe” la kimaslahi ya kivyama “lisituoe”  Kitaalamu alikuwa ni msomi wa shahada ya Mawasiliano ya Umma aliyotunukiwa Chuo Kikuu cha Makerere nchini, Uganda.  Alijiunga na Jeshi la Polisi na kufanya kazi kwa mwaka mmoja kisha akaacha kazi , baadaye  alipangiwa kitengo cha Habari makao makuu ya Polisi na kufanya kazi kwa mwaka mmoja. Bada ya Polisi alijiunga na World Vision kama  Afisa Mawasiliano(Communication/Information Officer)  na kufanya kazi kwa miaka kama minne hivi akiwa Makao makuu Arusha na baadae akahamishiwa tawi la Dar es salaam.
Alipotoka World Vision akajiunga na MKURABITA,  ambapo alifanya kazi kwa muda usiozidi miaka miwili akaacha.
Baada ya kuacha MKURABITA, akafungua duka lake la “electronics” lipo Benjamin Mkapa Tower, opposite na Posta Mpya ghorofa ya kwanza. Baadaye akaafungua vituo vyake vya kuuzia mafuta Ludewa na ndipo akaanza harakati za kuingia kwenye siasa na kuchaguliwa kuwa mbunge mwaka 2010. Inasemekana alikuwa hapendelei  kuwa mwanasiasa, japo baba yake alikuwa mkongwe wa TANU.
Mpaka anafariki ameacha mke na watoto wa tatu wa kiume.
Deo (kushoto) akiwa na mmoja wa rafiki zake  Bw. Zitto Kabwe enzi za uhai wake


Kwa vijana wa kileo alibeba karisma ya “kutotekwa” na uchama kwenye kutetea maslahi ya wananchi kama viongozi wengine, hivyo anatujenga kwa “ombwe” la kimaslahi ya kivyama “lisituoe”  bali siku kama ya leo ndiyo alitutoka!
Kwa sisi WAUNGWANA ni HISTORIA ILIOJEE tutamkumbuka!


MAGAZETI YA LEO YAPO HAPA KWA AJILI YAKO!

Ebwana eeh!  Front Pages ya baaadhi ya magazeti ya leo  Oktoba 15, 2016 yapo hapa kwa ajili yako msomaji wangu.














Friday 14 October 2016

BREAK NEWS: ALLOCATION YA MKOPO KWA WALIOOMBA MWAKA WA MASOMO 2016/2017

 Hii ndio Batch ya kwanza ya majina yapatayo 3966
 Kutazama Bofya hapa







Toa comment yako kwa kile ulichokiona!

KWELI WEWE NI BABA WA TAIFA

Usiyoyajua kuwa MWL. JULIUS KAMBARAGE NYERERE yanayofanya kuwa na heshima nzito:
1.Alizaliwa tarehe 13/04/1922 Butiama na kufariki tarehe kama ya leo 14/10/1999 kule London.Ni Rais wa kwanza Afrika kuachia madaraka kwa hiari yake mwenyewe.
2.Ni Rais wa kwanza kuhama Ikulu na kwenda kuishi kwenye nyumba aliyoijenga kwa mkopo akiwa bado Raisi.
3.Ni kati ya Rais aliyekuwa analipwa mshahara mdogo duniani na pengine kati ya raisi aliyewahi kulipwa mshahara mdogo barani Afrika mpaka sasa.
4. Ni Mtanganyika wa kwanza kusoma chuo kikuu nchini Uingereza na Muafrika wa pili kupata Degree nje ya Afrika, akisomea English, Political Economy, Social Anthropology, British History, Economic History, Constitutional Law, and Moral Philosophy.
5. Ni kiongozi aliyeisaidia China kuingia Umoja wa Mataifa na hotuba yake maarufu akisema
kwamba,"Umoja wa Mataifa si serikali ya dunia bali ni sehemu ambayo dunia nzima inakutana,
kwahiyo kumtoa China katika umoja wa mataifa ni kumtoa kuwa sehemu ya dunia".
6. Ndio mwanzilishi wa harakati za kupinga ubaguzi wa rangi Afrika ya Kusini- Anti Apartheid Movement mwaka 1959 pamoja na Trevor Huddleston nchini Uingereza.
7. Ni mmoja kati ya waanzilishi wa Umoja wa Afrika, 1963.
8. Amezisaidia nchi nyingi za Afrika kupata uhuru kuliko mtu mwingine yoyote katika historia ya ukoloni, nchi hizo ni Zambia (1964), Malawi (1964), Botswana (1966), Lesotho (1966), Mauritius (1968), Swaziland (1968) and Seychelles (1976) na baadae 1975 (Mozambique), (Angola), 1980 (Zimbabwe), 1990
(Namibia) na 1994 (South Africa).
9. Mwaka 2009 alitajwa na raisi wa mkutano mkuu wa Umoja wa Mataifa kama "World Hero of Social Justice".
10. Amepokea shahada mbalimbali kutoka, University of Edinburgh (UK), Duquesne University (USA), University of Cairo (Egypt), University of Nigeria (Nigeria), University of Ibadan (Nigeria), University of Liberia (Liberia), University of Toronto (Canada), Howard University (USA), Jawaharlal Nehru University (India), University of Havana (Cuba), National University of Lesotho, University of the Philippines, Fort Hare University (South Africa),Sokoine University of Agriculture (Tanzania), and Lincoln University (PA, USA).
11. Alipokea Tuzo ya Order of José Marti Cuba 1975, Order of the Aztec Eagle (Collar) Mexico 1975, Order of Amílcar Cabral Guinea Bissau 1976, the Nehru Award for International Understanding in 1976, the Third World Prize in 1982, Order of Eduardo Mondlane
Mozambique 1983, the Nansen Medal for outstanding services to Refugees in 1983, Order of Agostinho Neto Angola 1985, Sir Seretse Khama SADC Medal 1986, Joliot-Curie Medal of Peace 1988, the Lenin Peace Prize in 1987, the International Simón Bolívar Prize in
1992, and the Gandhi Peace Prize in 1995, Statesman of the 20th century by the Chama Cha Mapinduzi 2000, Order of the Companions of O. R. Tambo (Gold) South Africa 2004, Royal Order of Munhumutapa Zimbabwe 2005, Most Excellent Order of the Pearl of Africa (Grand Master) Uganda 2005, Order of Katonga Uganda 2005, National Liberation Medal Rwanda 2009, National Liberation Medal Rwanda 2009, Campaign Against Genocide Medal Rwanda 2009, Order of the Most Ancient Welwitschi Mirabilis Namibia 2010, Tanzania Professional Network Award 2011, Order of Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Tanzania 2011, National Order of the Republic (Grand Cordon) Burundi 2012 and Order of Jamaica, Jamaica.
12. Mwaka 2007 Rais Yoweri Museveni wa Uganda alimpa tuzo ya Katongo, Medali ya juu kuliko zote ya Jeshi la Uganda kwa heshima ya upinzani wake dhidi ya ukoloni na serikali ya Idi Amin.
13. Mitaa, barabara, majengo, vituo, shule, vyuo na vitu vilivyopewa jina lake; Daraja la Nyerere-Kigamboni,Julius Nyerere University of Kankan, in Kankan, Guinea, Nyerere Drive,Gaborone (1.6 km) in Botswana, Nyerere Avenue, Mombasa (1.5 km)
and Nyerere Road, Kisumu (2 km) in Kenya, Julius Nyerere Street, Windhoek (1.1 km) in Namibia, Julius Nyerere Street, Durban (0.5 km) in South Africa, Nyerere Road, Kitwe (1.4 km) in Zambia, Julius Nyerere Way, Harare (1 km) in Zimbabwe, Julius Nyerere International Airport, Julius Nyerere International Convention Centre, Nyerere Day- Public Holiday 14/10, Nyerere Cup, Nyerere Road, Unguja, Zanzibar (6.5 km), Nyerere Secondary School in Mwanga District and J.K. Nyerere Secondary School in Moshi, Kilimanjaro Region, Mwalimu J. K. Nyerere Secondary School in Mbozi District, Mbeya Region, Nyerere Memorial School in Korogwe, Tanga Region, Nyerere High School Migoli in Iringa Region, Nyerere Secondary School in Unguja, Zanzibar, Mwalimu Nyerere Foundation, Mwalimu Nyerere Museum Centre and Mwalimu Nyerere Memorial Academy- Tanzania.
14. Baadhi ya vitabu alivyoviandika ni, Freedom and Unity (Uhuru na Umoja), Freedom and Socialism (Uhuru na Ujamaa), The Arusha
Declaration, Education for self-reliance, The varied paths to socialism, The purpose is man, Socialism and development, Freedom and Development (Uhuru Na Maendeleo), Ujamaa, Crusade for Liberation, Education for Self-Reliance, na Uongozi na Hatima ya Tanzania.
15. Pamoja na kujulikana kama - Baba wa Taifa la Tanzania, Nchi za Kusini mwa Afrika zinamtambua kama baba wa Ukombozi wa Nchi za Kusini.
16. Pamoja na kujua lugha ya Kiswahili na Kiingereza kwa Ufasaha - pia alikuwa akifahamu lugha ya Kigiriki na Kilatini.
17. Julius Nyerere ameandikwa kwenye kitabu cha Enyclopia kama mtu pekee duniani katika historia ya karne ya 21, aliyeweza kuwafanya watu wa makabila, dini, asili na historia tofauti kujiona kama watu wamoja.

NUKUU KUNTU: BUSARA ZA MWALIMU


Siku ya leo katika kukumbuka ya miaka 17 aliyotutoka Mwalimu Nyerere ni wasaa wa kutazama moja ya misimamo yake.
Mwalimu Nyerere

“Unyenyekevu ukizidi unazaa uoga, uoga huzaa unafiki na kujipendekeza, mwisho wake mauti”

CHEKI VIDEO MPYA YA DAVIDO FT TINASHE-HOW LONG

Mnigeria Dvido akiwa na mwanadada Tinashe,  video yao hii hapa.
           Kuitazama Bonyeza hapa
          Kuidownload Bonyeza hapa




Unakaribishwa kutoa comment yako kwa kile ulichokiona!

TUJIKUMBUSHE: RAIS MSTAAFU BENJAMIN WILIAM MKAPA AKITANGAZA KIFO CHA MWALIMU

Leo ni kumbukumbu ya miaka 17 ya kifo cha Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, tukiamini kwa mengi mazuri  aliyoyatenda ila kwa vitendo vyenye weledi pekee.
Mwalimu Nyerere(kushoto) na Rais wa awamu ya tatu, Ndugu Benjamin Mkapa

Kwa kukumbuka siku hii, nakuletea video ya Rais mstaafu enzi hizo mwaka 1999, ndugu Benjamin Wliiam Mkapa akitangaza tanzia hii.
    Bofya hapa kutazama 

“Argue, Don't Shout" Ya Mwalimu Nyerere Tuiishi Kwa Vitendo

Hii ni makala niliyokuwekea uisome hapa Oktoba 14, ila siku iliyofuata Oktoba 15, 2016  imepata nafasi kwenye gazeti la TanzaniaDaima
   
   
Na 
Peter C. Mmbaga

Ndiyo muda wangu wa kuingia “Giningi” na Wabasi  wenzangu ambao tunaamini kwenye mawazo ya  chanya pasipo kupepesa  macho, safari ya Giningi inahitaji ufunge mkanda kweli kweli na leo nipo njiani kuongea na  kumpa pongezi za  “kuondoka” zake mapema mbasi wangu katika fikra Mwalimu mkuu, Baba Makongoro  kwakuwa angebaki mpaka sasa angekuwa anaduwaa kama mimi na vile hapendi  kuonekana  kwenye   “maamuzi  ya umimi”,  anakuwa mpole tu.
Kumbuka kipindi kile wakisema  baadhi ya viongozi   waliokuwa wanafanya mambo  tofauti, yeye alitoa tamko gani? Kwenye kitabu chake cha “Uongozi wetu na Hatima ya Tanzania” anabaki kama mshauri tu, japo kutokana na hadhi yake ama “popularity” aliyokuwa nao asingesikilizwa na wananchi kweli, katika kukataza?
Aliwaachia uhuru wajitathimini  wenyewe, na uhuru ni mbaya sana, walipoona   mbasi wangu katika fikra  chanya hajaja juu wakaona sawa tu, mambo yanafanyika,  anajifanya haoni. Kumbe “mbasi” ulikuwa “unawachora” tu.
“Giningi yetu” ina raha yake huku yupo Baba wa maridhiano, mbasi wangu katika fikra, Mandela yeye anatabasamu tu anasema “Real leaders must be ready to sacrifice  all for the freedom of their people“ kwa tafsiri isiyo rasmi ni kuwa “ Vingozi wa kweli wanatakiwa wawe tayari kujitoa vilivyo kwa  uhuru wa wananchi”, naye namwangalia natabasamu  kwa kuwa kazi aliyoiamua  Rais JPM ni ngumu  sana kwakuwa  wapiga vita mfumo  mzuri wapo  na hasa watendaji, “We got a Long Way To Freedom” ila kwa imani atawatumbua tu!
Baba Makongoro bwana ananifurahisha sana akasema “Siku Wamarekani wakinisifia nimefanya kazi nzuri nitajiuliza kuwa nimekosea wapi?”  ndiyo kitu nilichompendea hasa kwa kauli hizi za kujiamini kwa nukuu nilyooina kwenye gazeti moja la kila siku miaka mitatu nyuma, ni kauli ya Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), chuo ambacho Mwalimu alikianzisha na mara kwa mara kufika hapo kwa ajili ya mijadala na wanafunzi kuhusu uhuru na maendeleo ya Afrika na dunia kwa ujumla, Bashiru Ally, anaamini Mwalimu anastahili  kupewa tuzo  lakini ananyimwa kutokana na kuyaudhi mataifa ya magharibi wakati aliongoza harakati za kudai haki za binadamu na uhuru wa mataifa ya Afrika. Huu ndiyo ushujaa tunaouhitaji Rais JPM piga kazi kwa haki na kweli usihitaji kusifiwa na watu wa nje ila tu angalia uhuru uwepo kama Baba Makongoro alivyoutoa. Mwalimu vijana wa leo sio wa kipindi kile  “pesa” inawanunua wanashindwa kutetea maslahi ya nchi,  hasa wasomi dira hawaileti , ukanijibu “pesa ni matokeo” kama ulivyoainisha kwenye kitabu chako cha cha “Ujamaaa na Kujitegemea” lakini Mwalimu sasa sivyo, nadhani wakati nao unabadilika, ila  wanaamini,  pesa ndilo lenye nguvu!
Sasa hivi wasomi wanaonekana shujaa  kwenye dimbwi la mfumo  huu wakuogopa kuhoji, vyuo vikuu vimepoa  vimenyamaza, nahisi huko ndiko ulipowasikia kwa mara ya kwanza   kina ndugu Lowassa, JK  na wengineo,   ila sasa wanaogopa  kuitwa wasaliti ni bora kuliko kuonekana mnyenyekevu kwao halafu kwenye jamii uonekane “Kamuzu”. Wazee wetu  ukiwauliza watakujibu enzi za kupigania uhuru walimwita   huyu mtu walimwitaje  "aliyeolewa na wazungu" aliwabania waafrika haki zao, ndiyo nyimbo iliyokuwa kwenye mchamchaka.
Kwanini nimesema hayo?  Nakumbusha raia wote  na viongozi wasaliti kwa machinga, boda boda, mama ntilie , wasakatonge , wasio na ajira ni bora uonekane umemsaliti rafiki yako anayetafuta  “ujiko” kwa njia ya  “matukio” kuliko kuitwa "umeolewa nao" na jamii ni mbaya sana,  lakini Mwalimu hao watu tunao?
Wewe mwenyewe ukasema “Unyenyekevu ukizidi unazaa uoga, uoga huzaa unafiki na kujipendekeza, mwisho wake mauti”
Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu J.K Nyerere

Baba Makongoro kuna walimu  wamekuwa  ‘maarufu” kwa kipindi hichi kubwa ni kumpiga mwanafunzi  wa kidato cha tatu mwezi huu uliotuaga, kuna kitu baba nimegundua Walimu wengi wanakwenda pasipo ‘passion”, lengo ni kupata mkopo ambao miaka ya karibuni imekuwa  kipaumbele kwa walimu ili kusaidia changamoto za elimu yetu, japo wanafunzi wa siku hizi ni watukutu kufikia hatua ya kuchanganywa na malezi na utandawazi ambao tumeupokea “negative” sana kwenye matumizi yake.
Mtoto  kupewa adhabu hatujakataa, ni moja ya kufunza baba, kama wewe ulifanya pale Chuo Kikuu Cha Dar Es Salaam kwa mmoja wa viongozi wetu kugoma akiwa  Rais wa serikali ya wanafunzi-Daruso  enzi zako  wakigomea kutopatiwa maziwa na siagi, kweli enzi zako “walikula bata”  mbasi wangu, leo hii wanasota watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu  “no mkopo”, kipaumbele kimeharibu kila kitu na wengi wanakimbilia huo ualimu,  tasnia nyingine baada ya miaka kumi wasomi wengi watakuwa kwenye  tasnia moja halafu wasio na “passion” japo sio wote ama tasnia zote lakini Je, hali itakuwaje?
Enzi zako mtu akisema mimi ni mwalimu hiyo heshima anayopewa  ni nzito lakini leo sielewi, thamani imepungua sijui kisa ni nini? Ndo maana misongo ya mawazo  inakuwa mingi sana hata kupiga wanafunzi.
Mimi kusema kula bata ni kweli kwasababu   habari  hii niliwahi  kuhadithiwa na “anko” wangu aliyesoma na ndugu Rais  mstaafu kijana wako, Jakaya  Kikwete pale Shule ya Tanga (Tanga  School) enzi zako  Mwalimu Mkuu wa fikra yakini,  juu ya elimu,chakula(asubuhi chai nzito), na usafiri wa  bure kwa gharama za Serikali.  Ila nyakati zinabadilika!
Wakati tunaendelea na maongezi yetu ya Kibasi zaidi huko “Ginigi yetu”  kuna  msomi  enzi zake Mwalimu  akaniuliza leo hii madaftari  yanauzwa  kwa shilingi ngapi  wanafunzi, vipi madawati shuleni?  Nikamwambia najua, wajua, akanijibu halafu tuna misitu mikubwa nchini?
 Baba Makongoro ulivyooondoka kuna mwana hip hop aliimba “wasomi wanakimbilia siasa, Je, nchi itajengwa na nani? Hata mimi najiuliza nchi itajengwa na nani? Sielewi!

Mwalimu alizidi  nitoa tongotongo katika kuandaa  na maswala mengine yenye maslahi kitaifa yasiyohitaji mgawanyiko wa itikadi na uchama  kwa kile  waingereza wanachosema “number do not lie” wakimaanisha  nambari haidanganyi kwa kufanya mambo kwa  “ tathmini onyeshi” moja ni moja na nane si saba, kwakumshangaa  Waziri mwenye dhamana ya Afya  kukinzana na  Makamu wa Rais, kuhusu upungufu  wa madawa kwenye bohari ya Taifa!
Nakamwambia Mwalimu neno “siasa” ni mwiba kwa wananchi si neno  zuri kulizungumza  japo Rais JPM anawapa matumaini kuwa utendaji wake kwa kiasi chake kuna tija imeonekana Mwalimu,  kabla hatujaendelea zaidi   nikatafakari kuwa  ujasiri ni pale unapojua "siasa" si tatizo bali tatizo ni picha na taswira iliyojengeka mtu kuwa "mwanasiasa" ndani ya jamii na jibu tunalo kwa utendaji mzuri wa viongozi wetu  ili kugeuza neno "politics is dirty game". Itabadilika tu hii hali, kama enzi zako Ualimu ulivyoheshimika leo hii unaonekana taaluma ya kawaida! Sisi wenyewe hatupendi Mwalimu.
Nikamwona kifkra shujaa wa India, Mahatma Ghandi na falsafa yake kuwa “I love your Christ but not your Christianity” nikimaanisha  serikali na vyama vya siasa  ni sehemu salama na sera zenye weledi lakini  walioko ndani yake ndiyo kuna kila aina ya ubaya,udhalimu, na siasa chafu japo kuna wasafi na wenye kweli daima. Naipenda sera weledi yenye utekelezaji, itikadi ninayo,na “imani” kwa  kiongozi na mwananchi  mwenye misingi fanikishi ya kuileta “Tanzania ninayoitamani”, si kauli za kutofautiana  za  “makaisari” wetu na sio  ushabiki wa chama. Haya yakifanikiwa mbona “siasa nyeupe” itaonekana na tuishi ili kumuenzi Baba wa Taifa na hilo ndilo kusudi lake, siku siku ya leo tutoe  “speech” za kumsifia ila  hizo  sifa zake ninyi kiuhalisia na kiutendaji  mnaziishi kwenye vyombo vya habari.
Watanzania ni wepesi wa kusahau kama  zao la “kuamua” litaleta watu makini, wazalendo,wenye dira elekevu, na misimamo binafsi   tutakuwa tumefikia kiwango kikubwa katika “mchakato” wa kujitambua na kuutambua ukweli na ule mtazamo wa siasa ni mchezo mchafu (politics is the dirty game) tukiishi ya Baba Makongoro na sio kuienzi siku yake bila matendo sio maneno. Hata  Baba Makongoro kwenye “mjadala” wetu hapendi hilo swala.
Alichopenda ni “Argue, Don’t shout” na hichi ndicho serikali inakinzana na vyama vya upinzani sana, kwasababu kila mmoja anatoa kinachojipendelea ila tukumbuke tunajenga moja, Tanzania yetu katika siku hii ya kumuenzi Baba wa Taifa sio kwa makelele na sifa kedekede bila kuishi aliyoyaishi!
Pumzika kwa amani Mkuu, muda mwingine tutatembeleana!

Description: https://ssl.gstatic.com/ui/v1/icons/mail/images/cleardot.gif

MAJINA YA WANAFUNZI WOTE WALIOCHAGULIWA SOKOINE UNIVERSITY OF AGRICULTURE KWA SELECTION YA PILI

 
                                                        Kutazama majina bofya hapa



Unaweza kuacha comment yako hapa kwa kile ulichokiona!

TCU WAACHIA SELECTION YOTE YA WANAFUNZI KUJIUNGA VYUO VIKUU MBALIMBALI TANZANIA KWA MWAKA WA MASOMO 2016/2017

                                                 
                                                               Bonyeza hapa kuangalia



Unakaribishwa kuacha comment yako kwa kile ulichokiona!

Thursday 13 October 2016

KAMA ULIIKOSA VIDEO YA DJ KHALED ALIWASHIRIKISHA MASTAA KIBAO, HII HAPA!


                                                Bonyeza hapa kutazama video hii
                                                Bonyeza hapa kudownload video hii




                     Unakaribishwa kuacha maoni yako kwa kile ulichokiona!

R&B: NGOMA MPYA YA MAROON 5 FT KENDRICK LAMAR-DON'T WANNA KNOW


                      Zaidi ya mwaka sasa hukusikia ngoma ya Maroon 5, hii hapa sasa.
                                             Bonyeza hapa kusikiliza ngoma hii
                                          Bonyeza hapa kuidownload ngoma hii




Unakaribishwa kutoa comment  yako kwa kile ulichokisikiliza!

GOSPEL: TAZAMA VIDEO YA BRO VICTOR MBAGGA-NGUVU ZANGU

Unataka kujua mwimbaji Victor Mbagga anajinasibu kuwa nguvu zake anazitoa wapi?
                                   Bonyeza hapa kutazama video hii
                                  Bonyeza hapa kudownload video hii



Ukishaicheki unakaribishwa kutoa comment yako hapo chini!

HIP HOP: CHEKI NGOMA ZA NARI MCEE HAPA

Fanya uwezalo kumsapoti Nari Mcee. 



Unakaribishwa kuacha comment yako hapo chini!

GOSPEL: VIDEO YA BRO VICTOR MBAGGA "NI FURAHA KUWA NA YESU"


                                                  Bonyeza hapa kutazama video hii
                                                  Bonyeza hapa kudownload video hii


                                         Unakaribishwa kuacha comment yako hapo chini!

Wednesday 12 October 2016

ETHIOPIA KUFANYA MAGEUZI MFUMO WA UCHAGUZI


Kansela Merkel akikamilisha ziara yake Afrika ameahidi kutoa mafunzo kwa maafisa wa polisi wa Ethiopia kuhusu namna ya kukabiliana na waandamanaji. Ametaka waandamanaji wapewe uhuru wa kuandamana na uhuru kwa wapinzani.
Waziri mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn amesema serikali yake inataka kufanya mageuzi ya mfumo wa uchaguzi, ambao kwa muda mrefu umeutenga upinzani na kuchangia kutokea kwa maandamano mabaya ambayo yamedumu kwa miezi kadhaa. Haya yanajiri wakati Kansela wa Ujerumani Angela Merkel akimaliza ziara yake nchini humo ambapo amesema waandamanaji waruhusiwe kuandamana.
Waziri mkuu wa Ethiopia Hailemariam Desalegn amewaambia wanahabari kuwa “kufuatia mfumo uliopo sasa wa uchaguzi nchini humo, asilimia 51 ya kura inatosha kutwaa ushindi wa viti vyote". Na sasa serikali yake inataka kufanya marekebisho ili kuhakikisha mfumo huo unabadilishwa ili watu wote wakiwemo wapinzani wawakilishwe bungeni.

Chini ya mfumo uliopo sasa, muungano wa Hailemariam ambao ndio unatawala, ulishinda viti vyote 546 vya ubunge katika uchaguzi mkuu, uliofanywa mwaka jana. Hii hapa kauli ya Hailemariam kuhusu suala, la demokrasia na usalama nchini mwake."Ethiopia imejitolea kukuza demokrasia.Ethiopia imejitolea kuwa na demokrasia ya vyama vingi kulingana na katiba yetu. na Ethiopia imejitolea kuhakikisha haki za binadamu zinalindwa. Lakini Ethiopia pia inapinga ghasia ya misimamo mikali au makundi yanayojihami kwa fujo".
Hailemariam aliyasema hayo baada ya kukutana na mgeni wake Kansela wa Ujerumani Angela Merkel, akimaliza ziara yake ya siku tatu barani Afrika, ambapo amesema demokrasia iliyoimarika inahitaji kuwepo na upinzani pamoja na uhuru wa vyombo vya habari. Ameitaka Ethiopia kuwapa uhuru waandamanaji bila ya ukandamizaji wa aina yoyote. Kando na kuhimiza serikali kufanya mazungumzo na upinzani, Merkel pia ameahidi kuwa, nchi yake itatoa mafunzo kwa maafisa wa polisi wa Ethiopia kuhusu namna ya kukabiliana na waandamanaji.

Akiwa Ethiopia, Kansela Merkel amemwambia mwenyeji wake Waziri Mkuu Desalegn kuwa waandamanaji waruhusiwe kuandamana na kuwa hatua yoyote ya vyombo vya usalama iwe kulingana na sheria. Kadhalika amesema wanaharakati wa upinzani na watetezi wa haki za kibinadamu wanapaswa kuwa na uhuru wa kutekeleza majukumu yao. Lakini Waziri Mkuu Hailemariam amepinga madai kuwa maafisa wa polisi walitumia mbinu za fujo dhidi ya waandamanaji, na kuahidi kuwa serikali yake itachunguza visa hivyo.
Wiki iliyopita, zaidi ya watu 50 waliuawa kwenye mkanyagano baada ya polisi kujaribu kuwatawanya waandamanaji. Hali iliyosababisha kuongezeka kwa maandamano zaidi, na kulazimisha serikali kutangaza hali ya hatari nchini humo mwote. 
Ethiopia imekumbwa na maandamano ya miezi kadhaa ambapo waandamanaji wanashinikiza kupatikana kwa uhuru wa kisiasa na haki ya kumiliki ardhi, huku wakilaumu serikali kwa kuendeleza utawala wa kimabavu.
Katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, watu 400 wamekufa nchini Ethiopia kutokana na maandamano hayo dhidi ya serikali. Hayo yamesemwa na makundi ya kutetea haki za kibinadamu pamoja na wanaharakati wa upinzani.

Jumatatu wiki hii, rais wa Ethiopia alitangaza bungeni kuwa sheria za uchaguzi zitafanyiwa marekebisho ili kuruhusu vyama vingi vya kisiasa na kuwapa nafasi wapinzani. Hata hivyo, matumizi ya mtandao yangali yamezimwa nchini humo, baada ya maandamano kuzidi kwa muda wa wiki moja ambapo pia waandamanaji walifanya uharibifu katika biashara na afisi za ubalozi wa nchi zinazofikiriwa kushirikiana na serikali.
Marekani na mataifa mengine yameitaka serikali ya Ethiopia kujizuia katika kukabiliana na waandamanaji huku maafisa wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa wakitaka uchunguzi huru ufanywe kuhusu matukio hayo katika eneo la Oromia.
Merkel amekamilisha ziara yake ya siku tatu katika nchi za Mali, Niger na Ethiopia yenye lengo la kuhimiza uimarishaji wa usalama ili kupunguza wimbi la wakimbizi. Ethiopia ni mojawapo ya nchi inayowahifadhi wakimbizi wengi duniani. Mamia ya maelfu ya wakimbizi hao wakitoka Somalia, Sudan Kusini na kwingineko. Sawa na Ujerumani ambayo.
Merkel pia inakumbwa na mzigo wa wakimbizi kwa sasa, ambapo takriban wakimbizi mioni moja waliingia Ujerumani tangu mwaka jana pekee.pia amefungua rasmi jingo jipya la Muungano wa Afrika ambalo pia litakuwa la baraza la amani na usalama. Jengo hilo lililopo Addis Ababa limejengwa kwa ufadhili wa yuro milioni 27 kutoka Ujerumani.


Chanzo: DW

.

KANSELA MERKEL AZINDUA JUMBA LA MWALIMU NYERERE ADDIS ABABA


Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amezindua jumba jipya makao makuu ya Umoja wa Afrika ambalo limepewa jina la rais mwanzilishi wa taifa la Tanzania, Mwalimu Julius Nyerere ambaye siku ya Oktoba 14, 2016 itakuwa kumbukumbuku ya kifo chake.
Jumba hilo ambalo jina lake kamili ni Jumba la Amani na Usalama la Julius Nyerere limejengwa kwa ufadhili kutoka Ujerumani.

Litakuwa makao ya idara ya Amani na Usalama ya AU na litatumiwa pia na maafisa wa kutoa tahadhari ya mapema kuhusu mizozo barani pamoja na kuratibu juhudi za kulinda amani za AU.
Ujenzi wa jumba hilo, ambalo ukubwa wake wa sakafu ni mita 13,500 mraba na linaweza kutumiwa na wafanyakazi 360, uligharimu euro 27 milioni.
Jumba hilo afisi za kufanyia kazi, vyumba vya mikutano vya kutumiwa na Baraza la Amani na Usalama, chumba cha kuratibia shughuli, maktaba na vyumba vya shughuli za pembeni.

Mwalimu Nyerere, ambaye alikuwa rais wa Tanzania hadi 1985, alikuwa mmoja wa viongozi waanzilishi wa Muungano wa Nchi za Afrika (OAU) ambao sasa ni Umoja wa Afrika (AU).
Alishiriki sana katika jitihada za kuendeleza bara la Afrika na kusaidia mataifa ambayo hayakuwa yamepata uhuru kujipatia uhuru wake.
Mwalimu Nyerere alipigania sana kumalizwa kwa ubabe wa Wazungu katika nchi za Rhodesia (sasa Zimbabwe), Afrika Kusini, na taifa la Kusini Magharibi mwa Afrika/Namibia (sasa Namibia).



Chanzo: BBC Swahili

10 HARSH “TRUTHS” NOT TO BE AVOIDED WHICH WILL MAKE YOU A BETTER


One medieval philosopher Saint Thomas Aquinas once said “There is no higher GOD than truth”, live truly who you and accepting truth whenever pour on you.
Medieval Philosopher, St.  Thomas Aquinas 
Life is a hard place and most of us can be forgiven for feeling we are on the losing end of it. The simple truth is no one has an easy ride; most of us have had some serious ups and downs along the way. Below are 10 harsh truths that will make you a better person;

1. Life isn’t fair
Of course life isn’t fair it never is. The challenge is to find someone who has had an easy life all the way through, they don’t exist. The sooner you except this fact the happier you’ll be.
2. The first step is the hardest
Well it may be. It is also good to reach outside our comfort zone from time to time. The problem with comfort zones is they get smaller and smaller with time. Reaching out, and doing something new, can revitalize us and make us more rounded people.

3. Good things don’t come quickly
There is the opposite adage that good things are worth waiting for. The reality is good things are happening all the time. Okay, you didn’t win the lottery this week, but the chances are lots of good things have happened to you, be they small and fleeting. Make a note of the good things that happen each week, you’ll be surprised.
 
4. Not everyone gives support
It would be very strange if they did because we are all made up of different personalities, values and have different points of view. It would be impossible to please everybody all the time, there will always be doubters. Never let these people stop you from going for your goals and passions. These are the very things that make you a better person.



5. You can’t always be in control
That’s the way the world is made up, there will always be things you have no control over. The boss has control over you; the Inland Revenue has control over you along with your wife or husband. This is life, live with it, but don’t let it stop you from reaching out for your aims.
6. You can only accomplish great things with taking risks
Risk taking is a part of life; any successful businessman will tell you this. If you’re not prepared to take risks you will have harder time accomplishing what you want in life.

7. You’ll be better off without people you currently care about
Yes that’s true. You’ll be better off because you won’t have to worry about a loved one, falling ill, dying, or falling out of love. However, would being on your own without all this responsibility make you happier? It seems unlikely as the precious things in life are people, not money or possessions.
8. Death is a part of life
Yes that is true. Live with it, and that is not supposed to be a pun. There’s things you can do to make losing a loved one a lot less distressing: make them a bigger part of your life right now. Little things like making that call or paying a flying visit to a friend you haven’t seen in a while. These things will make you a better person.



9. You are the only thing holding yourself back from greatness
Being negative will hold you back. Instead, focus on the positive things and be happy now.

10. Bad things happen to good people
That’s the nature of life, the good die young too. But the opposite is also true, the good have good things happen to them, and the good can live to ripe old age.