Showing posts with label MICHEZO. Show all posts
Showing posts with label MICHEZO. Show all posts

Saturday, 15 October 2016

SIMBA I KILELENI

Mchezo wa VPL kati ya Simba iliyokuwa mwenyeji wa Kagera Sugar umemalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa goli mbili kwa bila.
Magoli ya Simba yamefungwa na beki Mzarimu Yassin akiunganisha mpira wa kona uliopigwa na Shiza Kichuya katika dakika ya 44 na goli la pili likifungwa na Shiza Kichuya kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 75.
Ushindi huo unaiwezesha Simba kufikisha alama 23 katika michezo tisa iliyocheza, ikishinda michezo saba na kutoa sare miwili na ikiwa na mchezo mmoja mkononi, Kagera Sugar inasalia kuwa na alama 15 ikiwa katika nafasi ya tatu ya msimamo wa VPL.


LIST YA WACHEZAJI WANAOWANIA TUZO YA MCHEZAJI BORA AFRIKA, SAMATTA YUMO!

Nahodha wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Samatta yu miongoni mwa majina yaliyotangazwa  na shirikisho la soka Afrika CAF  katika list ya wachezaji 30 wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2016.
Mtanzania Mbwana Samatta ambaye ni mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa mwaka 2015 kwa wachezaji wanaocheza Ligi za ndani ya Afrika, safari hii amepata nafasi ya kuwania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa ujumla kwa mara ya kwanza akiichezea klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji.
List  nzima ipo hivi;
List ya majina 25 ya wachezaji wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa Afrika kwa wachezaji wanaocheza ndani ya Afrika.




Tuesday, 11 October 2016

HAPPY EARTHSRONG "SHUJAA" SIR BOB CHARLTON

Sir Bob Charlton enzi zake.
Leo bwana ndiyo “birthday”  ya shujaa Sir Robert "Bobby" Charlton alizaliwa  11 Oktoba  1937. Ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu wa Uingereza, Anajulikana kama mmojawapo wa viungo wa kati wenye uwezo wa hali ya juu wa muda wote. Nembo muhimu katika timu ya taifa ya Uingereza ambapo alishinda Kombe la Dunia na Ballon d'O r mwaka 1966. Yeye alicheza karibu muda wote katika klabu yake  ya Manchester United, ambapo alikuwa mashuhuri kwa uwezo wake wa kushambulia na kupiga mashuti yaliypachikwa jina "Long Lange Shot" yaliyopigwa toka umbali mrefu. Alionywa kwa kadi mara mbili tu katika maisha yake ya soka; mara moja dhidi ya Argentina mwaka 1966 katika Kombe la Dunia, na katika mechi ya ligi kuu dhidi ya Chelsea. Alizaliwa huko Ashington, Northumberland. Charlton alicheza mechi yake ya kwanza kwa Manchester United katika kikosi cha kwanza mwaka 1956, na zaidi ya misimu miwili alipata nafasi ya uhakika katika timu. Ni moja ya wachezaji walionusurika katika ajali ya anga mjini Munich mwaka 1958 baada ya kuokolewa na Harry Gregg, baada ya kuisaidia timu ya Mashetani Wekundu kushinda kombe la Football League mwaka 1965 pia alishinda Kombe la Dunia na medali katika timu ya taifa ya Uingereza mwaka 1966 na kombe la “Football League” akiwa na Mashetani Wekundu mwaka uliofuata. Mwaka 1968 akiwa nahodha wa Manchester United alishinda Kombe la Ulaya akifunga mabao mawili katika mechi ya fainali . Amefunga mabao zaidi kwa United (249) kuliko mchezaji mwingine yeyote na kutokea kuwa mfungaji bora England wa muda wote  wa timu ya Taifa kwa mabao 49  na Wayne  Rooney kumpiku juzi kati kwa goli 50 katika mechi 107 alizocheza.


Hivyo kuanzia Mei 1968 hadi Septemba 2015, kwa Rooney kuvunja rekodi hiyo ndani ya Uingereza. Bobby Charlton alikuwa na rekodi ya kucheza mechi nyingi kwa Manchester United (758), kabla ya kuzidiwa na Ryan Giggs. Aliichezea Uingereza mara nne katika Kombe la Dunia (1958, 1962, 1966, na 1970), na kuisaidia Uingereza kushinda shindano hilo mwaka 1966.
Sir Bob Charlton siku za karibuni
Wakati wa kustaafu kwake kutoka timu ya England mwaka 1970, alikuwa ameichezea timu ya Taifa mechi nyingi kuliko mchezaji yeyote (mara 106 katika ngazi ya juu) ila Wayne Rooney kaivunja kwa mechi 107, kwa aliyocheza  mwaka jana dhidi ya Uswisi. Rekodi hii tangu wakati huo ilikuwa kwa upande wa Bobby Moore na Peter Shilton. Aliondoka Manchester United na kuwa meneja wa Preston North End katika msimu wa 1973-1974. Ambapo alikuwa mchezaji-meneja na baadaye kuwa mkurugenzi wa Wigan Athletic, Msimu uliofuata akawa mwanachama wa bodi ya wakurugenzi Manchester United tangu mwaka 1984 mpaka sasa msimu wa 2016/17.


Huyu ndiye Sir Robert "Bobby" Charlton aliyeshikilia rekodi ya ufungaji wa mabao Uingereza kwa miaka 47, HAPPY BIRTHDAY LEGEND!



Unakaribishwa kuacha comment yako hapo chini!

KINDA WA MIAKA KUMI ALA MKATABA JUVE

Kinda Rasheed Al Hajjawi
Mabingwa hao wa Italia, Juventus wamemchukua “kinda”  mpalestina Rasheed Al Hajjawi mwenye miaka 10, baada ya kuzungumzwa sana kwenye “media: za kiarabu siku za karibuni.   Licha ya kukulia mjini Gaza, “kinda” huyo alizaliwa na kukulia Norway.

Habari za kunaswa kwa kinda huyo zimekuja baada ya “skauti ya kisasa” ya kunyaka matukio, habari na vipaji ya mtandao wa kijamii kupitia Youtube, huku wakibashiri kuwa ni Lionel Messi mpya. ndani ya wiki ya karibuni  siku ya Jumanne pia kumetokea dogo mwingine kwa jina la Karamoko Dembele mwenye miaka 13, aliyefanya "appearance"  kwa dakika 10 za mwisho kwenye mechi ya Celtic U20's katika ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Hearts.

Dembele akiingia uwanjani 

DOGO SI WA MCHEZOMCHEZO
Kweli si wa mchezomchezo kabla ya kutua alishaibuka kwenye mazoezi ya klabu ya Liverpool, na pia kuwa karibu na mastaa wa Real Madrid.
Dogo Rasheed akiwa Liverpool

Kwenye mtandao wa “facebook”  dogo kazitundika picha za mastaa kadhaa aliopiga nao stori.

 
Dogo akiwa na kocha wa Real Madrid, Zinedine Zidane


Sunday, 2 October 2016

DAR DERBY SIO SEHEMU YA KUCHEZEA HISIA ZA WATU

Na
Gilbert Nchimbi, SJMC
+255 657 215 404

Mpira wa miguu ni mchezo unaopendwa na watu wengi sana duniani kwa hapa Tanzania, klabu kubwa za Simba na Yanga zina mashabiki wengi mno ndio maana uwanja unajaa sana zikikutana.

Hawa  watu wakikusanyika pale Uwanja wa taifa sio kama kuna sehemu wanalipwa, sio kama wanakodiwa mabasi kwenda kwenye ule mkusanyiko kama ambavyo tumezoea kuona kwenye mikutano ya siasa, mara huyu kapewa fulana huyu kapewa khanga,  huyu kapewa kofia,  huyu kakodiwa basi ili afike kwenye mkutano lakini kwenye mpira ni tofauti wale watu uliowaona pale uwanja wa taifa kushuhudia pambano la simba na yanga hawajakodiwa gari jumamosi ya jana  wala hawalipwi kufika kuona ile mechi cha zaidi wale ndio huwa wanalipa pesa zao kuingia pale uwanjani yaani kinachowapeleka pale ni mapenzi na hisia zao walizonazo juu ya timu zao watu wanazipenda hizi timu watu wanapoteza fahamu kwa ajili ya hizi timu watu wamepoteza maisha sababu ya Simba na Yanga.

Sasa mnavyoleta masihara na hisia za watu wale pale uwanjani kwa kutuwekea marefarii ambao wanashindwa kusimamia sheria kumi na saba za huu mchezo wa soka kuna hatarisha sana maisha ya wapenzi wa huu mchezo tuwe makini na waamuzi makosa yao yanapelekea amani kuvurugika uwanjani watu wanashindwa kuvumilia zingatieni sana huu mchezo mpira wa miguu ni zaidi ya mchezo,  mpira wa miguu ni maisha watu wanahitaji haki itendeke ili waishi kwa amani. Ni zaidi viti mia mbili kuharibiwa na baadhi ya watu kujeruhiwa hiyo jana.

Tusitake yanayotokeaga kwenye mechi za watani wa jadi kwenye nchi za wenzetu yatokee nchini kwetu ndo tuanze kulizingatia hili.

Tuesday, 20 September 2016

TOURE KUSTAAFU TIMU YA TAIFA KWA MALUMBANO YA WAKALA WAKE NA PEP

Yaya Toure
Itakuwa sio stori nzuri kwa kiungo wa Man city na timu ya taifa ya Cote d'Ivore, mkongwe Yaya Toure kustaafu kuitumikia timu yake ya taifa na zawadi ya kukaa "benchi" ya maneno isiyo ya "kifundi" toka kwa meneja wake Pep Gurdiola.
Toure mwenye miaka 33 ametoa tamko leo nakusema "Ni maamuzi magumu kuyachukua ila waache wachezaji wengine wapate nafasi, nawashakuru kwa sapoti mliyotoa mashabiki wangu".
Huku anatangaza kustaafu balaa ni kuwa kocha wake wa Man city, Pep Guardiola kaeleza kuwa hatocheza mechi yoyote mpaka aombe msamaha kutokana na kauli za wakala wake.
Wakala wa Toure, Dimitri Seluk zaidi ya wiki moja iliyopita alidai "Kama atachukua taji la Ligi ya Mabingwa msimu huu, basi nitasafiri mpaka England na nitasema mbele ya luninga kwamba Pep Guardiola ni meneja bora kabisa duniani,” Seluk alinukuliwa na gazeti la Sunday Mirror.
Wakala huyo alizidi kung'aka kuwa ni wakati sahihi kwa mchezaji huyo kung’oa nanga kwenye kikosi hicho kwenye dirisha la usajili mwezi wa kwanza, pia ni ukandamizaji uliokikuka misingi kwa mteja wake kuwekwa nje hasa akiwa ni mchezaji aliyeibeba vilivyo Man City. 
Sasa joto ya jiwe ipo kwa wakala wa Toure kujibu nakusema "si anataka (Pep) vita, atavipata...........anatakiwa amwombe msamaha Joe Hart, hawezi kumtoa mchezaji mwenye heahima yake England".
wakala wa Toure, Seluk(kushoto) na Yaya Toure

Dimitri ameyajibu hayomuda usiopungua masaa mawili mpaka matatu nakukazia zaidi yeye(Pep) ndio aombe msamaha kwa Toure kumuweka kwa benchi.
Toure aliyekuwemo kwenye kikosi cha "tembo" kilichochukua kombe la mataifa Afrika mwaka 2015, amelichezea taifa hilo mechi 102 na kufunga magoli 19.
Toure anastaafu baada ya kutumika kwa miaka 14.

COURTOIS: NATAMANI KURUDI MADRID



Inawezekana kuwa ni stori kutovutiwa  na   wapenzi  na mashabiki wa Chelsea baada ya  golikipa wao mbelgiji Thibaut Courtois kuonyesha kuvutiwa na maisha ya Madrid hivyo kuonyesha moja kwa moja hafurahii 'life' la Stamford Bridge. Courtois alipiga “stori” na gazeti la Marca, la huko Uhispaniola nalo limevujisha nia ya “goalie” huyo kurejea La Liga mchezaji alietengeneza jina  vyema Atletico Madrid kabla ya kutua Chelsea, amefunguka kuwa Madrid ni kama nyumbani hivyo ana hamu ya kuwepo mara nyingine.
Kwenye 'interview' na gazeti hilo alisema “Atletico ni klabu ya kifamilia, bado nawapenda”.
Alipohojiwa kuwa anataka kurudi Uhispaniola alidai “Ndio, kwasababu ya klabu hiyo(Atletico), na jinsi mji wa Madrid ulivyo na nchi nzima”



“Tokea mara ya kwanza nilipapenda Uhispaniola kwasababu ya watu wake, mtindo wa maisha,chakula…...bado “namaintain’ ulaji wao wa chakula, hata luninga zao nafuatilia……mimi ni nusu mhisipaniola’.
Kuhusu ratiba ya kurejea La Liga alisema “nina kandarasi ya misimu mitatu na Chelsea.  Mwaka 2008, mwaka wa mwisho wa kandarasi, nitapima kubaki au kuondoka”



RASHFORD KUWA KINDA ANAYELIPWA ZAIDI DUNIANI

Man United bado wanauguza vidonda vya kufugwa   3-1“wikendi” hii na Watford ila kuna kijana mdogo wa kujivunia ukiacha mastaa waliopo kikosini aliyefunga goli la pekee la United, ni kinda Marcus Rashford.
United wanatarajiwa “kuset” rekodi ya kandarasi nono ya pauni 50,000 kwa wiki mpaka 2020 pale  kandarasi yake ya sasa itakapokwisha ili kumfunga kuogopa “wanyemeleji”.
Hivyo, kijana mdogo tu mwenye miaka 18 anayetimiza miaka 19 mwezi ujao  anatarajia kuvunja rekodi ya dunia kuwa mchezaji  mdogo anayelipwa zaidi duniani kumfikia mreno  Renato Sanchez wa Byern Munchen. Alipewa kandarasi ya mwaka ya pauni milioni moja mwezi Mei baada ya kudumbukia kwenye soka la wakubwa mwezi wa pili na mpaka sasa amekuwa mfungaji mzuri toka mechi ya Europa alipofunga mara mbili dhidi ya FC Midtjylland na  alipokuwa na bosi Loius Van Gaal mpaka sasa akiwa bosi  mreno Jose Mourinho, hajageuka nyuma japo anatokea benchi kwa "aapearance"   gemu kadhaa.

Monday, 19 September 2016

ETI KILICHOMTOKEA CASILLAS KWA MOURINHO KIPO NJIANI KWA ROONEY?

Casillas(kushoto) na Mourinho.
 Ishu ya kutoogopa  na kuwa  "uso wa mbuzi" kwa mastaa huyu huyu kocha  Jose Mourinho  inatazamiwa kwa jicho la ajabu na mashabiki wa Man U. Inaelekea kilichomkuta Iker Casillas kwa kupigwa chini japo na ukongwe na heshima yake Madrid na kocha mwenye “vituko” Jose Mourinho kinaweza kutokea kwa Wayne Rooney akiwa na kocha huyo  ndani ya United.
Mashabiki wa United wanahisi Rooney anaweza kupigwa benchi na mwishowe kuuzwa kama vile Juan Mata.
Mourinho(kushoto) na Rooney.


Huo umekuwa utabiri wa mashabiki wengi kwenye mtandao wa “twitter” baada ya United kufungwa na Watford huku kiungo na nahodha huyo  kutofanya “tackling” na kupiga shuti “on target” na zaidi kutohusishwa kwenye kikosi kwenye  mechi ya Europa  dhidi ya Feyenoord ya Uholanzi.

Gundu kwa staa huyo aliyeshindwa kuibeba United kwa mechi Man City na Watford kwa kufungwa ukiachilia ambayo hakwenda Uholanzi dhidi ya Feyenoord,  uwezekano wa kupigwa chini ni rahisi kutokana na mawazo ya mashabiki hawa;