Inawezekana kuwa ni stori kutovutiwa na wapenzi na mashabiki wa Chelsea baada ya golikipa wao mbelgiji Thibaut Courtois kuonyesha kuvutiwa na maisha ya Madrid hivyo kuonyesha moja kwa moja hafurahii 'life' la Stamford Bridge. Courtois alipiga
“stori” na gazeti la Marca, la huko Uhispaniola nalo limevujisha nia ya “goalie”
huyo kurejea La Liga mchezaji alietengeneza jina vyema Atletico Madrid kabla ya kutua Chelsea, amefunguka kuwa Madrid ni kama nyumbani hivyo ana hamu ya kuwepo mara nyingine.
Kwenye 'interview' na gazeti hilo alisema “Atletico
ni klabu ya kifamilia, bado nawapenda”.
Alipohojiwa kuwa anataka kurudi Uhispaniola alidai “Ndio, kwasababu
ya klabu hiyo(Atletico), na jinsi mji wa Madrid ulivyo na nchi nzima”
“Tokea mara ya kwanza nilipapenda Uhispaniola kwasababu ya
watu wake, mtindo wa maisha,chakula…...bado “namaintain’ ulaji wao wa chakula,
hata luninga zao nafuatilia……mimi ni nusu mhisipaniola’.
Kuhusu ratiba ya kurejea La Liga alisema “nina kandarasi ya
misimu mitatu na Chelsea. Mwaka 2008,
mwaka wa mwisho wa kandarasi, nitapima kubaki au kuondoka”
No comments:
Post a Comment