Monday 19 September 2016

ICJ YAANZA KUISIKILIZA KESI YA MPAKA KATI YA KENYA NA SOMALIA

Mahakama  ya  Kimataifa  ya  Haki  (ICJ)  inayoungwa  mkono  na  Umoja  wa  Mataifa  imeanza  kusikiliza  kesi  ya  kugombea  mpaka  kati  ya  nchi  za  Kenya  na  Somalia  mjini  The  Hague  nchini  Uholanzi, ambapo  mwanasheria  mkuu  wa  Kenya  Profesa  Githu  Muigai  amesema  ataongoza  jopo  la  mawakili  na  maofisa  wa  ngazi  za  juu  kutoka  nchini    Kenya   ili  kuitetea  nchi  hiyo.
Mwanasheria Mkuu wa Kenya, Profesa Githu Muigai.
 Aidha  mwanasheria  huyo  wa  Kenya  amesema  kuwa  Kenya  inataraji kuituhumu Somalia  katika  kesi  hiyo  kwa  kuvunja  mkataba  wa  mwaka  2009  ambapo  amesema nchi  hizo  zilikubaliana  kutatua  mzozo  huo  unaohusisha  sehemu  za  nchi  hizo  ndani  ya  Bahari  ya  Hindi  kupitia  mazungumzo.  Eneo  hilo  linalogombaniwa  lina  ukubwa  wa  kilomita  za  mraba  42,000  na  linasadikiwa  kuwa  na  utajiri  wa  mafuta  na  gesi.

Katika  mgogoro  huo  Somalia  inataka  mpaka  wake  wa  baharini  uendelee  kwa  kufuata  mstari  wa  mpaka  ulio  nchi  kavu  unaolekea  kusini  mashariki  mwa  nchi  hiyo  wakati  Kenya  nayo  ikitaka  mpaka  huo  uwekwe  kwa  kufuata  mstari  usiopinda  unaoelekea  mashariki,  hali  hiyo  imesababisha  kutengeneza  umbo  la  pembetatu  kutokana  na  madai  ya  nchi  hizo  mbili  za  Afrika  Mashariki. Kesi  hiyo inataraji  kudumu  kwa  wiki  moja  ili  kutoa  mwelekeo  wa  namna  nchi  hizo  zitavyofikia  maridhiano. 
Kesi hiyo iliwasilishwa ICJ tangu Agosti, 2014.




No comments:

Post a Comment