Tuesday 20 September 2016

MLIPUKO MFULULIZO MAREKANI HUENDA IKAWA NA SURA YA UGAIDI

Wakati wachunguzi wa shirika la kijasusi la Marekani  FBI, mjini New York wakifuatilia ushahidi  ili kubaini   chanzo  cha  bomu lililolipuka katika eneo la Chelsea huko Manhattan siku ya Jumamosi usiku na kifaa cha pili ambacho hakikulipuka kilichopatikana eneo hilo, shirika hilo  la FBI pia  limesema linachunguza bomu lingine lililopuka katika jimbo la New Jersey saa chache kabla yakutaka kuongea na waandishi wa habari.
Agenti maalum wa FBI, Richard Thornton.
Mlipuko huo ambao ulitokea saa chache kabla ya "agenti" maalum wa FBI kuhusu tukio hilo, Richard Thornton kuzungumza na waandishi wa habari, alidai “kwa sasa tunafanya uchunguzi wa awali kama ni gaidi, nasema uchunguzi wa awali kwasababu kuna vitu vingi hatufahamu, hatufahamu kama shambulio hili linahusisha kikundi gani cha ugaidi, hivyo ndivyo uchunguzi ulipofikia”

Katika tukio hilo lilotokea eneo la Chelsea watu 29 wamejeruhiwa na tayari watu hao wameruhusiwa kuondoka hospitalini baada ya matiba huku maofisa hao wa FBI wakisema kuwa wanachunguza madai ya kundi la Islamic State yakuwa mtu mmoja aliekuwa amevalia mavazi ya kiaskari mwenye asili ya Somalia na kuendesha shambulizi kwa kutumia kisu na kuwajeruhi watu nane ndani ya duka la Crossroads Center mall, jimbo la Minnesota nchini marekani siku ya hiyo hiyo ya Jumamosi ni mfuasi wao.


No comments:

Post a Comment