Man United bado wanauguza vidonda vya kufugwa 3-1“wikendi”
hii na Watford ila kuna kijana mdogo wa kujivunia ukiacha mastaa waliopo
kikosini aliyefunga goli la pekee la United, ni kinda Marcus Rashford.
United wanatarajiwa “kuset” rekodi ya kandarasi nono
ya pauni 50,000 kwa wiki mpaka 2020 pale
kandarasi yake ya sasa itakapokwisha ili kumfunga kuogopa “wanyemeleji”.
Hivyo, kijana mdogo tu mwenye miaka 18 anayetimiza
miaka 19 mwezi ujao anatarajia kuvunja
rekodi ya dunia kuwa mchezaji mdogo anayelipwa
zaidi duniani kumfikia mreno Renato Sanchez wa Byern Munchen. Alipewa kandarasi ya mwaka
ya pauni milioni moja mwezi Mei baada ya kudumbukia kwenye soka la wakubwa
mwezi wa pili na mpaka sasa amekuwa mfungaji mzuri toka mechi ya Europa
alipofunga mara mbili dhidi ya FC Midtjylland na alipokuwa na bosi Loius Van Gaal mpaka sasa akiwa bosi mreno Jose Mourinho, hajageuka
nyuma japo anatokea benchi kwa "aapearance" gemu kadhaa.
No comments:
Post a Comment