Tuesday 20 September 2016

RASHFORD KUWA KINDA ANAYELIPWA ZAIDI DUNIANI

Man United bado wanauguza vidonda vya kufugwa   3-1“wikendi” hii na Watford ila kuna kijana mdogo wa kujivunia ukiacha mastaa waliopo kikosini aliyefunga goli la pekee la United, ni kinda Marcus Rashford.
United wanatarajiwa “kuset” rekodi ya kandarasi nono ya pauni 50,000 kwa wiki mpaka 2020 pale  kandarasi yake ya sasa itakapokwisha ili kumfunga kuogopa “wanyemeleji”.
Hivyo, kijana mdogo tu mwenye miaka 18 anayetimiza miaka 19 mwezi ujao  anatarajia kuvunja rekodi ya dunia kuwa mchezaji  mdogo anayelipwa zaidi duniani kumfikia mreno  Renato Sanchez wa Byern Munchen. Alipewa kandarasi ya mwaka ya pauni milioni moja mwezi Mei baada ya kudumbukia kwenye soka la wakubwa mwezi wa pili na mpaka sasa amekuwa mfungaji mzuri toka mechi ya Europa alipofunga mara mbili dhidi ya FC Midtjylland na  alipokuwa na bosi Loius Van Gaal mpaka sasa akiwa bosi  mreno Jose Mourinho, hajageuka nyuma japo anatokea benchi kwa "aapearance"   gemu kadhaa.

No comments:

Post a Comment