Saturday 3 September 2016

HISTORIA ILIOJEE: NDUGU CLEOPA DAVID MSUYA



Ni HISTORIA ILIOJEEE, Mtanzania pekee aliyabahatika kuteuliwa  kwa kofia ya waziri mkuu na marais wawili tofauti, hapa namaanisha  Baba wa Taifa mwl. Julius  Kambarage Nyerere pamoja na  Rais wa awamu pili ndugu Alli Hassani Mwinyi,  si mwingine ni ndugu Cleopa David Msuya .
Mara ya kwanza ilikuwa ni siku 13 baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 1980 wa chama kimoja, ambapo kama kawaida mnapotoka uchaguzini, moja ya kazi za kwanza ya Rais ni kumtangaza Waziri Mkuu, na ndipo hapa November 07, 1980 Mwl. Julius Nyerere akamtangaza Cleopa Msuya kuwa Waziri mkuu. huyu ndiye ndugu Cleopa David Msuya aliyezaliwa novemba 4, 1931, huko wilayani Mwanga, tarafa ya Usangi katika kijiji cha Chomvu mkoani Kilimanjaro.
Ni kizazi cha wasomi wa Chuo Kikuu cha Makerere toka mwaka 1952 mpaka 1955,  ndugu Msuya  aliyeanza kwa utumishi wa  sekta ya umma, maendeleo ya vijiji toka mwaka 1956 hadi 1964. Kuanzia mwaka 1964 alihudumu kama katibu kiongozi kwenye wizara tofauti tofauti ikiwemo wizara ya maendeleo ya jamii na utamaduni kutoka mwaka 1964 hadi 1965, wizara ya makazi na maendeleo ya maji kati ya mwaka 1965 mpaka 1967, 1967 mpaka 1970 ilihudumu kwenye wizara ya uchumi na mipango na baadaye akahamishiwa wizara ya fedha toka mwaka 1970 hadi 1972.
Februari mwaka 1972 aliteuliwa kuwa waziri wa fedha mpaka mwaka 1975 aliula tena kuiongoza wizara ya viwanda na biashara  hadi mwaka 1983, alipoteuliwa kwa mara ya kwanza kushika wadhifa wa kuwa waziri mkuu.
Alipoteuliwa kuwa Waziri Mkuu na  Makamu wa pili wa Rais, ndugu Msuya hakumaliza awamu yote kwani  mnamo Februari 24, 1983 alibadilishwa na nafasi yake kuchukuliwa na Hayati Edward Sokoine ambaye naye hakumaliza awamu ile kwani alifariki mwaka mmoja tu baadaye yaani April 12, 1984.
Awamu  pili ndugu  Msuya aliteuliwa kuwa Waziri Mkuu Desemba, 1994 alipoteuliwa na Rais Ali Hassani Mwinyi kupokea  nafasi ya John Malecela ambaye alijiuzulu siku mbili kabla ya uteuzi huu wakati kikao cha NEC-CCM, kikiendelea. Hivyo kutokana na katiba kuruhusu akawa Waziri Mkuu na Makamu wa kwanza wa Rais wa jamhuri ya Muungano.
 Hapo nyuma mnamo mwaka 1992, nchi yetu iliingia katika mageuzi makubwa ya mfumo wa kisiasa pale ilipoamua kufuata mfumo wa vyama vingi vya siasa. Mabadiliko haya yalisababisha Katiba ya nchi ifanyiwe mabadiliko ili kuruhusu mfumo huu wa demokrasia ya vyama vingi ufanye kazi nchini ambapo nafasi mbalimbali za uongozi pia ziliguswa na mabadiliko hayo hivyo mwaka 1994, kufuatia mfumo wa demokrasia ya vyama vingi kuruhusiwa nchini ilijitokeza haja ya kuifanyia mabadiliko nafasi ya Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ili iweze kukidhi mageuzi haya ya kisiasa. Ilionekana kwamba katika mfumo huu mpya wa demokrasia ya vyama vingi si rahisi tena kuwa na Makamu wa Rais wawili kama ilivyokuwa wakati wa mfumo wa demokrasia ya chama kimoja hivyo ndugu Cleopa mwana  David  ndiye  aliyemalizia rojo ya tamu na shubiri ya kuwa na vyeo viwili vikubwa kwa wakati mmoja.
Nafasi alizokuwa nazo aliziacha kwenye uchaguzi mpya wa kihistoria wa vyama vingi uliofanyika kwa mara ya kwanza mwa 1995, na baadaye kuteuliwa kuwemo kwenye bunge maalum la katiba nafasi aliyodumu nayo hadi kustaafu mwaka 2000. Alipata nafasi ya kuwa nwenyekiti wa kilimanjaro gvt forum mwaka 2006.
Hadi kustaafu kwake ameeendelea kuwa kada mwaminifu wa chama cha mapinduzi hadi hii leo.

Ni HISTORIA ILIOJEE kwetu sisi WAUNGWANA  kumgusia  ndugu Cleopa Msuya ambaye kipekee mpaka sasa ndiye Waziri Mkuu wa kwanza Tanzania kupitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano kwa mtindo wa sasa kuthibitishwa na Bunge na pia kushika vye vikubwa awamu mbili  yaani   Waziri mkuu kikiongozana na Makamu wa Pili wa Rais wa  Jamhuri na baadaye Waziri  Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais kwa wakati mmoja kwasababu ni  HISTORIA ILIOJEEE!!!!

No comments:

Post a Comment