Tuesday 20 September 2016

TOURE KUSTAAFU TIMU YA TAIFA KWA MALUMBANO YA WAKALA WAKE NA PEP

Yaya Toure
Itakuwa sio stori nzuri kwa kiungo wa Man city na timu ya taifa ya Cote d'Ivore, mkongwe Yaya Toure kustaafu kuitumikia timu yake ya taifa na zawadi ya kukaa "benchi" ya maneno isiyo ya "kifundi" toka kwa meneja wake Pep Gurdiola.
Toure mwenye miaka 33 ametoa tamko leo nakusema "Ni maamuzi magumu kuyachukua ila waache wachezaji wengine wapate nafasi, nawashakuru kwa sapoti mliyotoa mashabiki wangu".
Huku anatangaza kustaafu balaa ni kuwa kocha wake wa Man city, Pep Guardiola kaeleza kuwa hatocheza mechi yoyote mpaka aombe msamaha kutokana na kauli za wakala wake.
Wakala wa Toure, Dimitri Seluk zaidi ya wiki moja iliyopita alidai "Kama atachukua taji la Ligi ya Mabingwa msimu huu, basi nitasafiri mpaka England na nitasema mbele ya luninga kwamba Pep Guardiola ni meneja bora kabisa duniani,” Seluk alinukuliwa na gazeti la Sunday Mirror.
Wakala huyo alizidi kung'aka kuwa ni wakati sahihi kwa mchezaji huyo kung’oa nanga kwenye kikosi hicho kwenye dirisha la usajili mwezi wa kwanza, pia ni ukandamizaji uliokikuka misingi kwa mteja wake kuwekwa nje hasa akiwa ni mchezaji aliyeibeba vilivyo Man City. 
Sasa joto ya jiwe ipo kwa wakala wa Toure kujibu nakusema "si anataka (Pep) vita, atavipata...........anatakiwa amwombe msamaha Joe Hart, hawezi kumtoa mchezaji mwenye heahima yake England".
wakala wa Toure, Seluk(kushoto) na Yaya Toure

Dimitri ameyajibu hayomuda usiopungua masaa mawili mpaka matatu nakukazia zaidi yeye(Pep) ndio aombe msamaha kwa Toure kumuweka kwa benchi.
Toure aliyekuwemo kwenye kikosi cha "tembo" kilichochukua kombe la mataifa Afrika mwaka 2015, amelichezea taifa hilo mechi 102 na kufunga magoli 19.
Toure anastaafu baada ya kutumika kwa miaka 14.

No comments:

Post a Comment