Winga wa Madrid mwenye manjonjo yake Christiano
Ronaldo anahusishwa na “stori” mpya yakuwa “penzini” na mrembo Desire Cordero,
ambaye ashawahi kuvikwa taji la Miss Spain siku za nyuma.
Hilo limeripotiwa na gazeti la udaku la
uhispania la Corazon Czn katika toleo lao jipya.
Wawili hao wameripotiwa kuwa pamoja sasa
yapata mwezi mmoja na mrembo huyo kuhusishwa tayari kashaingia mjini Madrid
kufanya “makazi” yake.
Hili ndilo gazeti la "Corazon Czn" lililoripoti kwa kichwa kikisema "LA PAREJA SORPRESA DEL ANO" kwa tafsiri isiyo rasmi ikimaanisha "SUPRISE, WAPENZI WAPYA" na mstari wa chini "LLEVEN VIENDOSE UN MES"- "YAPATA MWEZI SASA"
No comments:
Post a Comment