Tuesday 20 September 2016

TRUMP: KUMPA MATIBABU YA KISIASA GAIDI NI UDHAIFU KWA SERIKALI

Mgombea wa Democratic, Donald Trump
Akizungumza   mjini   Fort Myers  katika  jimbo  la  Florida  nchini  Marekani  Bwana  Donald Trump  amesema  kuwa   hatua  ya  serikali  ya  nchi  hiyo  inayoongozwa  na chama  cha  Democratic  kumpatia  matibabu  ya  kisasa  mshukiwa  wa  ugaidi  ni  ishara  ya  dhahiri   kuwa  kuna  udhaifu  mkubwa  ndani  ya  idara  ya  usalama  wa  taifa  ya  nchi  hiyo,  Bwana  Trump  alisema ‘’Sasa  tumemfanyia  ukarimu   wa  ajabu  sana,  ametibiwa  na  miongoni  mwa  madaktari  bora  duniani,  amepelekwa  kwenye  hospitali  ya  kisasa  na  amepewa  chumba  cha  kisasa  hospitalini  hapo  na  huenda  atapokea  huduma  zote  akiwa  humo,  ukizingatia  jinsi nchi  hii  ilivyo’’. Bwana  Ahmad  Khan  Rahami  wenye  umri  wa  miaka  28  ambaye  ni  mzaliwa  wa  Afghanistan  anatuhumiwa  kufanya  mashambulizi  ya  kigaidi  katika  miji  ya  New  York  na  New  Jersey  nchini  Marekani  jumamosi  iliyopita  ambapo  tayari  amefunguliwa  mashtaka  matano  ya  kujaribu  kutekeleza  mauaji.
Mshukiwa wa mlipuko miwili mfufulizo New York na New Jersey, Ahmad Rahmani Khan
Mgombea  urais  wa  Republican  nchini  Marekani  Bwana  Donald  Trump  ameelezea  masikitiko  yake  kuhusu  namna  serikali  ya  nchi  hiyo  ilivyomkarimu  mshukiwa  wa  vitendo  vya  kigaidi   katika  jiji  la  New  York  jumamosi  iliyopita   Bwana Ahmad Khan Rahami  ambapo  maofisa  wa  serikali  wanadaiwa  kumpatia  matibabu  mshukiwa  huyo  na  kisha  kumpatia  wakili  atakayemtetea  wakati  atakapopandishwa  kizimbani  kwa  tuhuma  za  ugaidi.

No comments:

Post a Comment