Monday 19 September 2016

ETI KILICHOMTOKEA CASILLAS KWA MOURINHO KIPO NJIANI KWA ROONEY?

Casillas(kushoto) na Mourinho.
 Ishu ya kutoogopa  na kuwa  "uso wa mbuzi" kwa mastaa huyu huyu kocha  Jose Mourinho  inatazamiwa kwa jicho la ajabu na mashabiki wa Man U. Inaelekea kilichomkuta Iker Casillas kwa kupigwa chini japo na ukongwe na heshima yake Madrid na kocha mwenye “vituko” Jose Mourinho kinaweza kutokea kwa Wayne Rooney akiwa na kocha huyo  ndani ya United.
Mashabiki wa United wanahisi Rooney anaweza kupigwa benchi na mwishowe kuuzwa kama vile Juan Mata.
Mourinho(kushoto) na Rooney.


Huo umekuwa utabiri wa mashabiki wengi kwenye mtandao wa “twitter” baada ya United kufungwa na Watford huku kiungo na nahodha huyo  kutofanya “tackling” na kupiga shuti “on target” na zaidi kutohusishwa kwenye kikosi kwenye  mechi ya Europa  dhidi ya Feyenoord ya Uholanzi.

Gundu kwa staa huyo aliyeshindwa kuibeba United kwa mechi Man City na Watford kwa kufungwa ukiachilia ambayo hakwenda Uholanzi dhidi ya Feyenoord,  uwezekano wa kupigwa chini ni rahisi kutokana na mawazo ya mashabiki hawa;

No comments:

Post a Comment