Monday 19 September 2016

NANGAA: UCHAGUZI MKUU CONGO HADI MWAKANI

Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Joseph Kabila.
Pamoja na mkutano  wa  upatanishi ulioongozwa  na  aliyekuwa  mwenyekiti  wa  umoja  wa  Afrika  Bwana  Edem  Kodjo  uliofanyika  nchini  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo mwanzoni  mwa  mwezi  Septemba  mwaka  huu  kati ya wapinzani na serikali ya nchi hiyo inayoongozwa na Rais Joseph Kabila.  Tume ya Uchaguzi ya Jamhuri  ya  Kidemokirasia  ya  Kongo   imesisitiza   kuwa  hakuna  uwezekano  wa  uchaguzi  kufanyika  nchini  humo  mwaka  huu  kama ilivyoelezwa kwenye katiba  ya  nchi  hiyo.

Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi ya nchi hiyo ambayo ilitarajiwa kuanza mchakato wake wa kufanyika kwa uchaguzi kuanza jumatatu ya wiki hii, Bwana Corneille Nangaa amesema suala hilo kwa sasa haliwezekani na badala yake anashauri uchaguzi ufanyike mwaka ujao.




Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi, Corneille Nangaa.
Kufuatia  tamko  hilo  hali  si  shwari  ndani  ya  miji  mikubwa  ya  Jamhuri  ya  Kidemokrasia  ya  Kongo  ambapo  makundi  ya  upinzani  yamefanya  mkaandamano  makubwa  katika  miji  ya  nchi  hiyo  ikiwemo  Kinshasa  na  Kivu  pamoja  na  maeneo  mengine  ili  kuishinikiza  tume  ya  uchaguzi  ya  nchi  hiyo  itengue  uamuzi  huo  na  kuruhusu  uchaguzi  ufanyike  mwaka  huu  kwa  mujibu  wa  katiba

No comments:

Post a Comment