Mgombea wa Republican, Bw. Donald Trump |
Sasa anapendekeza kuwa wafanyiwe
majaribio ya matumizi ya dawa, kabla ya kufanyika kwa mjadala wao wa mwisho
hapo siku ya Jumatano ya wiki hii.
Katika mkutano wake wa hivi punde
uliofanyika New Hampshire, Bwana Trump kwa mara nyingine, amedai kuwa kuna
njama za kumuibia kura.
Timu ya kampeini ya Bi Clinton,
imesema kwamba wapigaji kura, sasa wameona bayana kile anachokiita juhudi za
aibu za Bwana Trump za kutaka kuhujumu shughuli za upigaji kura.
Trump, anazidi kudidimia katika
majimbo mengi, huku akikabiliwa na madai ya udhalilishaji wanawake kingono.
Chanzo: BBC Swahili
Chanzo: BBC Swahili
No comments:
Post a Comment