Shirika la ndege la Kenya Airways limeahirisha
safari zake tano za kwenda ndani na nje ya nchi leo October 16 2016 kutokana na
upungufu wa Wahudumu wa ndege kazini.
Taarifa inasema sababu hasa ya kuahirisha safari hizo tano za Mombasa, Kilimanjaro,Juba, Maputo, Harare na Lusaka ni
kutofika kazini kwa Wahudumu wa ndege ambao wamepangiwa zamu kwa wakati huo.
Imeelezwa kuwa baadhi ya Wafanyakazi wa shirika hilo hawajaripoti
kazini toka Ijumaa iliyopita ambapo shirika linaendelea kufatilia kujua chanzo
ni nini na jinsi ya kutatua tatizo na Mwajiri.
Kwa utaratibu ndege za abiria huwa na masharti yake kwenye kila
safari ikiwa ni pamoja na kuwa na namba flani ya idadi ya Wahudumu ndani ya
ndege ambayo ni lazima itimie, sasa kutokana na Wahudumu wa Kenya Airways kuwa
wachache imebidi ndege nyingine zisisafiri.
Chanzo: Millardayo
Chanzo: Millardayo
No comments:
Post a Comment