Mwanamuziki wa Congo, Koffi Olomide ambaye Julai
mwaka huu aliwasili Nairobi Kenya kwa ajili ya shoo na
baadae kuripotiwa kukamatwa kwa tuhuma za kumshambulia “dancer” wake wa kike ni
baada ya kusambaa kwa video iliyomuonyesha akifanya kitendo hicho. Baada
ya kupita miezi kadhaa tangu kutokea kwa tukio hilo na Koffi Olomide kutowahi
kujitokeza hadharani kulizungumzia, amejitokeza kupitia kipindi cha TV
cha Churchill Show, baada ya kupita miezi mitatu amewaomba msamaha wakenya
na mashabiki wake kwa ujumla n kunukuliwa akisema
’Kupitia Churchill
show, nataka kusema na nyinyi na kutuma ujumbe wa upendo, heshima na urafiki,
mimi nasikitika kwa kile kilichotokea na maombi yangu nisamehewe kwa kile
kilichotokea, mimi ni mwanadamu tu licha kwa kuwa ni maarufu’:- Koffi
Olomide
No comments:
Post a Comment