Monday, 5 September 2016

WASANII WAMEPOKEA VIBAYA STORI YA LIL WAYNE KUACHA MUZIKI


Mpaka sasa wasanii na mashabiki kibao wamepokea stori hizo kwa huzuni wakiwemo  Missy Elliott, Lupe Fiasco, Chevy Woods,  Flying Lotus, na wengineo, Mkali Liltunechi ameamua hilo baada ya kuona muziki wake umeandamwa na matatizo kibao.
Aliandika kwenye Twitter: "Sasa sijiwezi tena, sipo poa kiakili, na naondoka kwa staha na nashukuru mashabiki wangu."

Hata hivyo, hajafafanua iwapo ataacha sekta ya uimbaji kabisa, au ataacha tu uimbaji wa muziki wa kufoka. Mwanamuziki huyo wa umri wa miaka 33 hata hivyo amesema hataki "kuonewa huruma".
Lil Wayne amekuwa akigonga vichwa vya habari hivi karibuni kwa visa mbalimbali,  huku rapa Rick Ross akionekana kujibu maneno ya shabiki  aliyehitaji Tunechi kusainiwa Maybach Music Group(MMG) kwa kuandika “Muunganishe Birdman kwenye simu”

Amekuwa na mzozo wa muda mrefu na  lebo ya Cash Money Records inayomilikiwa na babaye kimuziki Birdman, kuhusiana kucheleweshwa kwa albamu yake ya 11, ambayo imepewa jina Tha Carter V. Alishutumu kampuni hiyo siku mbili zilizopita akitumbuiza na Drake mjini Miami.
Polisi Miami walifika nyumbani kwake kisiwa cha La Gorce baada ya mtu kupiga simu 911 akisema kulikuwa na ufyatuaji risasi. Habari hizo hazikuwa za kweli.


Hii ndio “tweet”  ya Lil Wayne;
 Lil Wayne WEEZY FVerified account‏@LilTunechi
I AM NOW DEFENSELESS AND mentally DEFEATED & I leave gracefully and thankful I luh my fanz but I'm dun

Hawa ni kati ya wasanii walioguswa;

 Missy Elliott ‏@MissyElliott  @LilTunechi Prayers up 4 whatever u may be enduring right now this to will pass & may u find PEACE  I will always be a fan of your work


Chris Clemons ‏@chrisclemons91
@LilTunechi       The game will never be the same!!! Long live the  of my generation.


WASANII WAMEPOKEA VIBAYA STORI YA LIL WAYNE KUACHA MUZIKI


Mpaka sasa wasanii na mashabiki kibao wamepokea  kwa huzuni stori ya mkali wa rap mwenye vionjo vya mziki vilivyozaa vijana kadhaa kama Future, YG, na Young  Thug kuwa ameacha muziki. Wakali kibao waizungumzia "ishu" hiyo  huzuni, wakiwemo  Missy Elliott, Lupe Fiasco, Chevy Woods,  Flying Lotus, na wengineo, Mkali Liltunechi ameamua hilo baada ya kuona muziki wake umeandamwa na matatizo kibao.
Aliandika kwenye akaunti yake ya twitter: "Sasa sijiwezi tena, sipo poa kiakili, na naondoka kwa staha na nashukuru mashabiki wangu."

Hata hivyo, hajafafanua iwapo ataacha sekta ya uimbaji kabisa, au ataacha tu uimbaji wa muziki wa kufoka. Mwanamuziki huyo wa umri wa miaka 33 hata hivyo amesema hataki "kuonewa huruma".
Lil Wayne amekuwa akigonga vichwa vya habari hivi karibuni kwa visa mbalimbali,  huku rapa Rick Ross akionekana kujibu maneno ya shabiki  aliyehitaji Tunechi kusainiwa Maybach Music Group(MMG) kwa kuandika “Muunganishe Birdman kwenye simu”

Amekuwa na mzozo wa muda mrefu na  lebo ya Cash Money Records inayomilikiwa na baba yake kimuziki Birdman, ishu kubwa ni kuhusiana na kucheleweshwa kwa albamu yake ya 11, ambayo imepewa jina Tha Carter V. Alishutumu kampuni hiyo siku kadhaa zilizopita akitumbuiza na Drake mjini Miami.
balaa lingine ni la hivi juzi kati baada ya polisi wa  Miami kufika nyumbani kwake kisiwa cha La Gorce baada ya mtu kupiga simu 911 akisema kulikuwa na ufyatuaji risasi. Habari hizo hazikuwa za kweli.


Hii ndio “tweet”  ya Lil Wayne;
 Lil Wayne WEEZY FVerified account‏@LilTunechi
I AM NOW DEFENSELESS AND mentally DEFEATED & I leave gracefully and thankful I luh my fanz but I'm dun

Hawa ni kati ya wasanii walioguswa;

 Missy Elliott ‏@MissyElliott  @LilTunechi Prayers up 4 whatever u may be enduring right now this to will pass & may u find PEACE  I will always be a fan of your work


Chris Clemons ‏@chrisclemons91
@LilTunechi       The game will never be the same!!! Long live the  of my generation.


Sunday, 4 September 2016

MOURINH0 KAMGEUKA SCHWEINSTEIGER

Ilionekana kama mvumilivu hula mbivu kwa  kiungo Bastian Schweinsteiger baada ya kocha wa Man U, Jose Mourinho  kuonyesha kutomhitaji  ila kiungo  alikaza na kuonekana shujaa mbele ya “special one”  siku chache baada ya jina lake kujumuishwa kwenye kikosi cha Man United kwenye msimu wa ligi wa 2016-17,  ila balaa limekuja baada ya Bastian Schweinsteiger kugeuziwa kibao na kocha wake Mourinho baada ya jina lake kutojumuisha katika kikosi kitakachoshiriki Ligi ya Europa. Schweinsteiger ambaye huko nyuma alicheza kwa mafanikio makubwa kunako klabu ya Bayern Munich ameichezea Ujerumani michezo 121.
Kiungo huyo mkongwe amestaafu soka la kimataifa  baada ya Jumatano  iliyopita kufanyiwa sherehe ya kuagwa kwenye Timu ya Taifa ya Ujerumani maarufu kama Die Manschaft kufutiwa kufanyika mchezo maalum dhidi ya Finland na kushinda mabao 2-0.
Katika kikosi hicho, viungo 10 wametajwa huku jina la Schweisteiger likipigwa panga.
Kikosi kizima kipo hivi:
Makipa: David De Gea, Sergio Romero, Sam Johnstone
Mabeki: Eric Bailly, Phil Jones, Marcus Rojo, Daley Blind, Chris Smalling, Luke Shaw, Timothy Fosu-Mensah, Antonio Valencia, Matteo Darmian, Axel Tuanzebe
Viungo: Paul Pogba, Juan Mata, Jesse Lingard, Michael Carrick, Ashley Young, Ander Herrera, Henrikh Mkhitaryan, Marouane Fellaini, Morgan Schneiderlin, Memphis Depay
Washambuliaji: Wayne Rooney, Zlatan Ibrahimovic, Anthony Martial, Marcus Rashford.


BECKHAM: MWACHENI ROONEY MPAKA ATAKAPOONA HAWEZI

Nahodha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya England, David Beckham ameweka hilo wazi baada ya kuona staa Wayne Rooney wengi wakimzungumzia kuwa ni muda kumpumzika kwa sasa.
Beckham ambaye aliichezea kwa mafanikio ya wastani timu ya taifa kuliko klabu alizopita alituma jumbe hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram kuelekea mechi dhidi ya Slovakia ambapo Rooney anakwenda kuvunja rekodi ya kucheza mechi nyingi ndani ya timu ya taifa leo usiku.
"Cheza mpaka muda utapofika huwezi tena......hakuna hisia unazopata ukiwa unacheza kwaajili ya Taifa lako ukiwa Wembley" alidai David Beckham.
Wayne Rooney kwa miezi ya karibuni ameonekana hayuko 'fit' na hasa wadau wakiona ni nafasi ya kipekee kuwaachia makinda waliopo.
Mshambuliaji nyota na nahodha wa Uingereza Wayne Rooney anatarajia kustaafu soka la kimataifa baada ya kumalizika kwa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 itakayofanyika nchini Urusi.
Kwa upande wake akihojiwa Rooney ambaye amefunga mabao 53 katika mechi 115 kwa Uingereza, amesema pindi Kombe la Dunia la Urusi litakapomalizika anadhani wakati wake wa kuaga soka la kimataifa utakuwa umefika.
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa michuano hiyo itakuwa nafasi yake ya mwisho kufanya kila kitu na Uingereza hivyo bado ataendelea kufurahia miaka miwili iliyobakia.
Kama Rooney akicheza mchezo wa Jumapili hii wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Slovakia, atakuwa amevunja rekodi ya David Beckham ya kucheza mechi nyingi katika timu ya taifa.
Soma ujumbe  wa Beckham hapo chini kupitia mtandao wa Instagram:
" So tonight Wayne becomes England’s most capped outfield player .. I keep listening to people say Wayne should stop playing for his country to prolong his club career .. Wayne should retire from playing for his country… Seriously .. As a player you retire when you’re ready.. Representing you’re country is the highest level you can reach as a professional player , walking out in an England shirt at Wembley is one of the greatest feelings as a player you can ever have … Don’t let anyone take that away from you .. Every kid around the world that loves this game dreams of walking out in the national team colours and representing the country they love .. Continue till you can’t give anymore .. Congratulations mate @manchesterunited @england”.
David Beckham na Wayne Rooney mwenye jezi no.10 kiindi wakiiwa wote timu ya  taifa

BECKHAM: MWACHENI ROONEY MPAKA ATAKAPOONA HAWEZI

Nahodha huyo wa zamani wa timu ya taifa ya England, David Beckham ameweka hilo wazi baada ya kuona staa Wayne Rooney wengi wakimzungumzia kuwa ni muda kumpumzika kwa sasa.
Beckham ambaye aliichezea kwa mafanikio ya wastani timu ya taifa kuliko klabu alizopita alituma jumbe hiyo kupitia ukurasa wake wa Instagram kuelekea mechi dhidi ya Slovakia ambapo Rooney anakwenda kuvunja rekodi ya kucheza mechi nyingi ndani ya timu ya taifa leo usiku.
"Cheza mpaka muda utapofika huwezi tena......hakuna hisia unazopata ukiwa unacheza kwaajili ya Taifa lako ukiwa Wembley" alidai David Beckham.
Wayne Rooney kwa miezi ya karibuni ameonekana hayuko 'fit' na hasa wadau wakiona ni nafasi ya kipekee kuwaachia makinda waliopo.
Mshambuliaji nyota na nahodha wa Uingereza Wayne Rooney anatarajia kustaafu soka la kimataifa baada ya kumalizika kwa michuano ya Kombe la Dunia mwaka 2018 itakayofanyika nchini Urusi.
Kwa upande wake akihojiwa Rooney ambaye amefunga mabao 53 katika mechi 115 kwa Uingereza, amesema pindi Kombe la Dunia la Urusi litakapomalizika anadhani wakati wake wa kuaga soka la kimataifa utakuwa umefika.
Nyota huyo aliendelea kudai kuwa michuano hiyo itakuwa nafasi yake ya mwisho kufanya kila kitu na Uingereza hivyo bado ataendelea kufurahia miaka miwili iliyobakia.
Kama Rooney akicheza mchezo wa Jumapili hii wa kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Slovakia, atakuwa amevunja rekodi ya David Beckham ya kucheza mechi nyingi katika timu ya taifa.
Soma ujumbe  wa Beckham hapo chini kupitia mtandao wa Instagram:
" So tonight Wayne becomes England’s most capped outfield player .. I keep listening to people say Wayne should stop playing for his country to prolong his club career .. Wayne should retire from playing for his country… Seriously .. As a player you retire when you’re ready.. Representing you’re country is the highest level you can reach as a professional player , walking out in an England shirt at Wembley is one of the greatest feelings as a player you can ever have … Don’t let anyone take that away from you .. Every kid around the world that loves this game dreams of walking out in the national team colours and representing the country they love .. Continue till you can’t give anymore .. Congratulations mate @manchesterunited @england”.
David Beckham na Wayne Rooney mwenye jezi no.10 kiindi wakiiwa wote timu ya  taifa

MAMA THERESA WA CALCUTTA ATANGAZWA KUWA MTAKATIFU

Maelfu ya watu wameshuhudia kwa pamoja ambapo Papa Francis amemtangaza mtawa Mama Teresa kuwa mtakatifu.
Mwanamama huyo wa Albania ambaye alifariki mwaka wa 1997 alianzisha shirika la hisani la kimishenari ili kuwasaidia wasionacho katika mtaa wa mabanda wa Calcutta nchini India.
Hivyo kuanzia sasa ataitwa mtakatifu Teresa wa Calcutta.
Waandishi na wataalamu wa mambo wanasema kuwa maisha yake yanaenda sambamba na maono ya Papa Francis kuhusu kanisa linalojikakamua kuwasaidai watu masikini.
Lakini wakosoaji wanasema kuwa Mama Teresa hakuwasaidia watu waliokuwa wagonjwa na alilaumiwa kwa kujaribu kuwabadilisha dini watu masikini wa kabila la Hindu nchini India kuwa Wakristo.
 Mama Theresa

TAIFA STARS HAINA REKODI DHIDI DHIDI YA SUPER EAGLE

Taifa Stars imeshindwa kuvimba ili kuitafuta rekodi iliyowekwa na Wanaigeria katika mechi nane za kimataifa walizokutana.
Mchezo wa jana uliochezwa uwanja wa Akwa Ibom huko Nigeria, ulikuwa wa mwisho  wa kundi G katika hatua za kufuzu AFCON 2017 huko Gabon dhidi ya Super Eagles, mchezo ulikwisha huku mshambuliaji kijana  wa Man City, Kelechi Iheanacho akitupia dakika ya 77.
Kwa goli hilo ndoto za Taifa Stars iliyokuwa ikiongozwa na nahodha wake Mbwana Samatta anayekipiga klabu ya Genk ya huko Ubelgiji ziliishia kuambulia historia ya sare ya mechi tatu na kufungwa mechi tano(ya jana ikiwemo) hivyo hakuna  "ubabe" wowote kwa Taifa Stars dhidi ya Super Eagle iliyoongozwa na kiungo mkongwe Mikel Obi na mshambuliaji machachari Ahmed Mussa. 

Mafarao wa Misri ni kati ya waliopenya ndani ya kundi la G.