Sunday 4 September 2016

MAMA THERESA WA CALCUTTA ATANGAZWA KUWA MTAKATIFU

Maelfu ya watu wameshuhudia kwa pamoja ambapo Papa Francis amemtangaza mtawa Mama Teresa kuwa mtakatifu.
Mwanamama huyo wa Albania ambaye alifariki mwaka wa 1997 alianzisha shirika la hisani la kimishenari ili kuwasaidia wasionacho katika mtaa wa mabanda wa Calcutta nchini India.
Hivyo kuanzia sasa ataitwa mtakatifu Teresa wa Calcutta.
Waandishi na wataalamu wa mambo wanasema kuwa maisha yake yanaenda sambamba na maono ya Papa Francis kuhusu kanisa linalojikakamua kuwasaidai watu masikini.
Lakini wakosoaji wanasema kuwa Mama Teresa hakuwasaidia watu waliokuwa wagonjwa na alilaumiwa kwa kujaribu kuwabadilisha dini watu masikini wa kabila la Hindu nchini India kuwa Wakristo.
 Mama Theresa

No comments:

Post a Comment