Monday 5 September 2016

WAKALA WA YAYA AMBWATUKIA PEP GUARDIOLA

Kiungo Yaya Toure akiwa na wakala wake, Dimitri Seluk(kushoto)
Dimitri Seluk ni wakala ambaye  sio maarufu sana aliyedumu  kwa miaka 15 na  kiungo Muivory Coast Yaya Toure, ambaye kwake  ni zaidi ya baba kwani  Toure humwita “Papushka”  na aliamua kumpa heshima ya  jina lake kwa  kumwita mwanae wa mwisho, unajua balaa lake?
Zinaweza kuwa stori za kawaida  jinsi tunavyosonga mbele kutokana na mkongwe Bastian  Schweinsteigekuachwa  kwenye “list” ya watakaokuwepo kwenye ligi ya mabingwa na kocha wake Jose Mourinho ndani ya Old Trafford sasa upande wa mbili ndani ya mji wa Manchester, Man City, Msenegali Yaya Toure,aliyetimka Barcelona iilyokuwa chini ya Guardiola mwaka 2010 na kuhamia Man City, amebaki Etihad baada ya dirisha la usajili kufungwa rasmi na hivyo hana nafasi tena ya kushiriki Michuano hiyo ya Ligi ya Mabingwa.
Toure amwenye miaka 33 hajaingia kiwanjani kwenye mechi tatu za mwanzo wa msimu zaidi mechi moja ya  kuwania kufuzu kucheza makundi ya Ligi ya Mabingwa dhidi ya Steaua Bucharest  ya Guardiola, kitendo hicho kikamkera  wakala wake Dimitri Seluk  akaamua kumbwatukia Pep  kwa maneno ya shombo.
“Kama atachukua taji la Ligi ya Mabingwa msimu huu, basi nitasafiri mpaka England na nitasema mbele ya runinga kwamba Pep Guardiola ni meneja bora kabisa duniani,” Seluk alinukuliwa na gazeti la Sunday Mirror.
Wakala huyo  anadhani  ni wakati sahihi kwa mchezaji huyo kung’oa nanga kwenye kikosi hicho kwenye dirisha la usajili mwezi wa kwanza.
Wakala huyo anaona ni ukandamizaji uliokikuka misingi kwa mteja wake kuwekwa nje hasa akiwa ni mchezaji aliyeibeba vilivyo Man City. “Haya ni maamuzi ya Pep na tunapaswa kuyaheshimu. Yaya ni mchezaji mwenye weledi na hivyo basi anafanya kila kitu ambacho anaelekezwa kufanya” alidai
“Pengine maono ya  Pep, kwamba anafaa kucheza dakika 10 za mwisho za mchezo wa Kombe la Ligi dhidi ya timu ya daraja la tatu……….ndiyo, natania tu lakini” alinukuliwa wakala huyo


No comments:

Post a Comment