Serikali ya Somalia imesitisha kwa muda ndege zote zinazoingiza miraa
kutoka taifa jirani la Kenya.
Biashara hiyo ina
thamani ya mamia ya mamilioni ya madola kila mwaka.
Waziri wa maswala ya
anga nchini Somalia Ali Ahmed Jama Jangali,amesema kuwa marufuku hiyo itaanza
kutekelezwa siku ya Jumanne lakini hakutoa maelezo zaidi.
Miraa ni maarufu sana
nchini Somalia ,ambapo hutafunwa kwa saa kadhaa na hutumika kusisimua mwili .
Miraa mingi katika
sehemu ya kusini na katikati mwa Somalia hutoka nchini Kenya.
Haikuzwi nchini
Somalia.
Miraa hutumika na
imepigwa marufuku nchini Tanzania, Marekani pamoja na mataifa kadhaa ya Ulaya.
Chanzo:BBC Swahili
No comments:
Post a Comment