Ilionekana kama
mvumilivu hula mbivu kwa kiungo Bastian
Schweinsteiger baada ya kocha wa Man U, Jose Mourinho kuonyesha kutomhitaji ila kiungo
alikaza na kuonekana shujaa mbele ya “special one” siku chache baada ya jina lake kujumuishwa
kwenye kikosi cha Man United kwenye msimu wa ligi wa 2016-17, ila balaa limekuja baada ya Bastian Schweinsteiger
kugeuziwa kibao na kocha wake Mourinho baada ya jina lake kutojumuisha katika
kikosi kitakachoshiriki Ligi ya Europa. Schweinsteiger ambaye huko nyuma
alicheza kwa mafanikio makubwa kunako klabu ya Bayern Munich ameichezea
Ujerumani michezo 121.
Kiungo huyo mkongwe amestaafu soka la kimataifa baada ya Jumatano iliyopita kufanyiwa sherehe ya kuagwa kwenye
Timu ya Taifa ya Ujerumani maarufu kama Die Manschaft kufutiwa kufanyika mchezo
maalum dhidi ya Finland na kushinda mabao 2-0.
Katika kikosi hicho, viungo 10 wametajwa huku jina la
Schweisteiger likipigwa panga.
Kikosi kizima kipo hivi:
Makipa: David De Gea, Sergio Romero, Sam Johnstone
Makipa: David De Gea, Sergio Romero, Sam Johnstone
Mabeki: Eric
Bailly, Phil Jones, Marcus Rojo, Daley Blind, Chris Smalling, Luke Shaw,
Timothy Fosu-Mensah, Antonio Valencia, Matteo Darmian, Axel Tuanzebe
Viungo: Paul Pogba, Juan Mata, Jesse Lingard, Michael
Carrick, Ashley Young, Ander Herrera, Henrikh Mkhitaryan, Marouane Fellaini,
Morgan Schneiderlin, Memphis Depay
Washambuliaji: Wayne Rooney, Zlatan Ibrahimovic, Anthony
Martial, Marcus Rashford.
No comments:
Post a Comment