Wednesday, 12 October 2016

10 HARSH “TRUTHS” NOT TO BE AVOIDED WHICH WILL MAKE YOU A BETTER


One medieval philosopher Saint Thomas Aquinas once said “There is no higher GOD than truth”, live truly who you and accepting truth whenever pour on you.
Medieval Philosopher, St.  Thomas Aquinas 
Life is a hard place and most of us can be forgiven for feeling we are on the losing end of it. The simple truth is no one has an easy ride; most of us have had some serious ups and downs along the way. Below are 10 harsh truths that will make you a better person;

1. Life isn’t fair
Of course life isn’t fair it never is. The challenge is to find someone who has had an easy life all the way through, they don’t exist. The sooner you except this fact the happier you’ll be.
2. The first step is the hardest
Well it may be. It is also good to reach outside our comfort zone from time to time. The problem with comfort zones is they get smaller and smaller with time. Reaching out, and doing something new, can revitalize us and make us more rounded people.

3. Good things don’t come quickly
There is the opposite adage that good things are worth waiting for. The reality is good things are happening all the time. Okay, you didn’t win the lottery this week, but the chances are lots of good things have happened to you, be they small and fleeting. Make a note of the good things that happen each week, you’ll be surprised.
 
4. Not everyone gives support
It would be very strange if they did because we are all made up of different personalities, values and have different points of view. It would be impossible to please everybody all the time, there will always be doubters. Never let these people stop you from going for your goals and passions. These are the very things that make you a better person.



5. You can’t always be in control
That’s the way the world is made up, there will always be things you have no control over. The boss has control over you; the Inland Revenue has control over you along with your wife or husband. This is life, live with it, but don’t let it stop you from reaching out for your aims.
6. You can only accomplish great things with taking risks
Risk taking is a part of life; any successful businessman will tell you this. If you’re not prepared to take risks you will have harder time accomplishing what you want in life.

7. You’ll be better off without people you currently care about
Yes that’s true. You’ll be better off because you won’t have to worry about a loved one, falling ill, dying, or falling out of love. However, would being on your own without all this responsibility make you happier? It seems unlikely as the precious things in life are people, not money or possessions.
8. Death is a part of life
Yes that is true. Live with it, and that is not supposed to be a pun. There’s things you can do to make losing a loved one a lot less distressing: make them a bigger part of your life right now. Little things like making that call or paying a flying visit to a friend you haven’t seen in a while. These things will make you a better person.



9. You are the only thing holding yourself back from greatness
Being negative will hold you back. Instead, focus on the positive things and be happy now.

10. Bad things happen to good people
That’s the nature of life, the good die young too. But the opposite is also true, the good have good things happen to them, and the good can live to ripe old age.






HISTORIA ILIOJEE: BIBI TITI MOHAMED

Bibi Titi Mohamed

 Ni HISTORIA ILIOJEE! mwanamke jasiri, shujaa na mwenye msimamo, moja ya barabara kuu ndani ya jiji la Dar es Salaam, jina lake limo kwa heshima ya mchango wake mkubwa wa  kuleta uhuru wa Tanganyika.
Si mwingine ni Bibi Titi Mohamed,  mwanamama, aliyekuwa kiongozi  mmojawapo katika  harakati za kudai uhuru wa Tanganyika, baadaye aliongoza Umoja wa Wanawake wa Tanzania (UWT), chama cha wanawake katika chama cha Tanganyika African National Union (TANU), na baadaye akawa waziri wa wanawake na masuala ya kijamii katika serikali ya Mwalimu Nyerere.
Bi Titi  Mohamed alikuwa mwanamke wa Kiislamu aliyezaliwa jijini Dar es Salaam mnamo  mwaka 1926 na baba mfanyabiashara na mama mkulima. Alipata elimu ya shule za msingi pekee na alipofikisha  umri wa miaka 14 tu aliolewa na mume mzee.
Bi Titi Mohamed alipata nguvu  ya kuwa mwanaharakati   kupitia kipaji cha kuimba, enzi za ujana wake alikuwa mwimbaji mzuri wa kwasida na hivyo kuwa  kama mwimbaji kiongozi katika ngoma katika kikundi cha muziki na ngoma ambacho kilimwongozea uzoefu wa kuwa mbele ya umati.
Nguvu ya kushiriki katika majukumu ya uongozi na uhusiano ndani ya mitandao wanawake na mapambano ya kitaifa yallianza mwaka 1950, baada ya Vita Kuu ya II ya dunia, Tanganyika ikiwemo nchi  nyingine katika harakati za uzalendo zilikuwa zimeshika kasi. Mwaka 1954, TANU iliundwa chini ya uongozi wa mwalimu na  baadaye Rais Julius Nyerere. 
Bibi Titi na Mwalimu J.K Nyerere kwenye pozi enzi hizo
Muda si mrefu baadaye mwaka  1955, Bibi Titi alikasimishwa  kiti cha UWT, na ndani ya miezi mitatu ya uteuzi wake, walijiunga wanawake zaidi ya 5,000 kama wanachama wa TANU, na hivyo kwa mrengo huo wa  wanawake uliianzishwa na jukumu kubwa kwa mapambano ya uhuru na UWT kufanya kazi kubwa ya kukuza maadili  ya TANU kwa raia. Pia umoja wanawake ukapaza sauti moja katika mapambano dhidi ya ukoloni.
 Bibi Titi kupitia wanaharakati wanawake walikuwa na uwezo wa kutumia mitandao yao mbalimbali ya kijamii na kiuchumi kwa kuongeza fedha kwa kiasi kikubwa kwaajili ya chama cha  TANU. Zaidi ya hayo, Bibi Titi akiwa na kipawa cha  usemaji, yeye mwenyewe, alihamasisha wanawake kupitia makundi ngoma na kusimamia viongozi wao kuunda nafasi kwa ajili ya kushughulikia wanachama na kuwasaidia, pia  makundi hayo yalikuwa wazi kwa wanawake wote waliotaka kujiunga, na kuishia kuwa mitandao yenye nguvu  kisiasa ajili ya kubadilishana taarifa,  tangazo la mikutano ya kampeni na maandamano.

Mwishowe mafanikio yaliingia  mwaka 1961,  kwa Tanganyika kupata Uhuru. 
Bibi Titi Mohamed bahati mbaya kisiasa  ilimpata mwaka 1965 wakati alipopoteza kiti chake cha ubunge. Mwaka 1967, yeye alijiuzulu kutoka uwaziri .
Baadaye alipata masaibu ya kisiasa  kwa kiasi kikubwa ilifanya kutoweka katika maisha ya umma na  baadaye   mnamo   Novemba 5, 2000,  Bibi Titi Mohamed pumzi yake ilirejea ilipotoka katika  hospitali ya Net Care huko Afrika Kusini.
HISTORIA ILIOJEE inajivunia Bibi Titi, mwanamama wa shoka, malkia wa nguvu  atakumbukwa kwa mengi,  heshima yake  ipo kwenye kutoa mwanga wa harakati za wanawake dhidi ya mfumo  mibovu  kwenye kila nyanja ya maisha,  kwetu sisi  WAUNGWANA ni HISTORIA ILIOJEEE!




Unakaribishwa kuacha comment yako hapo chini!

JPM AWATAKA WATUMISHI KUREJESHA POSHO


Rais JPM amewataka Watumishi wa Umma walioalikwa katika kilele cha sherehe za Mwenge ambazo zitafanyika tarehe 14 Oktoba kutohudhuria na warudishe posho za safari walizolipwa. 
Viongozi waliotajwa kutakiwa kufuta safari zao za kwenda Bariadi ni pamoja na wakuu wote wa mikoa, wilaya, wakurugenzi wote wa  mamlaka za serikali za mitaa, mameya, na wenyeviti wote wa Halmashauri  za majiiji, manispaa, miji na wilaya pamoja na watumishi ambao huambatana nao wakiwemo madereva na wasaidizi wao ambao kwa idadi hufikia takribani 1,500.
Kwa kuwa sherehe za kilele cam bio za mwenge wa Uhuru huambatana na maandhimisho ya siku ya kumbukumbuku ya Baba wa Taifa, hayati, Mwalimu J.K  Nyerere aliyefariki miaka 17 iliyopita, agizo hilo limewataka viongozi wote wa mikoa na wilaya kubaki katika maeneo yao ya kazi na kujiwekea utaratibu wa jinsi ya kuienzi siku hiyo.

 Hii hapa ni “Press Release” ya taarifa hiyo.

Tuesday, 11 October 2016

HAPPY EARTHSRONG "SHUJAA" SIR BOB CHARLTON

Sir Bob Charlton enzi zake.
Leo bwana ndiyo “birthday”  ya shujaa Sir Robert "Bobby" Charlton alizaliwa  11 Oktoba  1937. Ni mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu wa Uingereza, Anajulikana kama mmojawapo wa viungo wa kati wenye uwezo wa hali ya juu wa muda wote. Nembo muhimu katika timu ya taifa ya Uingereza ambapo alishinda Kombe la Dunia na Ballon d'O r mwaka 1966. Yeye alicheza karibu muda wote katika klabu yake  ya Manchester United, ambapo alikuwa mashuhuri kwa uwezo wake wa kushambulia na kupiga mashuti yaliypachikwa jina "Long Lange Shot" yaliyopigwa toka umbali mrefu. Alionywa kwa kadi mara mbili tu katika maisha yake ya soka; mara moja dhidi ya Argentina mwaka 1966 katika Kombe la Dunia, na katika mechi ya ligi kuu dhidi ya Chelsea. Alizaliwa huko Ashington, Northumberland. Charlton alicheza mechi yake ya kwanza kwa Manchester United katika kikosi cha kwanza mwaka 1956, na zaidi ya misimu miwili alipata nafasi ya uhakika katika timu. Ni moja ya wachezaji walionusurika katika ajali ya anga mjini Munich mwaka 1958 baada ya kuokolewa na Harry Gregg, baada ya kuisaidia timu ya Mashetani Wekundu kushinda kombe la Football League mwaka 1965 pia alishinda Kombe la Dunia na medali katika timu ya taifa ya Uingereza mwaka 1966 na kombe la “Football League” akiwa na Mashetani Wekundu mwaka uliofuata. Mwaka 1968 akiwa nahodha wa Manchester United alishinda Kombe la Ulaya akifunga mabao mawili katika mechi ya fainali . Amefunga mabao zaidi kwa United (249) kuliko mchezaji mwingine yeyote na kutokea kuwa mfungaji bora England wa muda wote  wa timu ya Taifa kwa mabao 49  na Wayne  Rooney kumpiku juzi kati kwa goli 50 katika mechi 107 alizocheza.


Hivyo kuanzia Mei 1968 hadi Septemba 2015, kwa Rooney kuvunja rekodi hiyo ndani ya Uingereza. Bobby Charlton alikuwa na rekodi ya kucheza mechi nyingi kwa Manchester United (758), kabla ya kuzidiwa na Ryan Giggs. Aliichezea Uingereza mara nne katika Kombe la Dunia (1958, 1962, 1966, na 1970), na kuisaidia Uingereza kushinda shindano hilo mwaka 1966.
Sir Bob Charlton siku za karibuni
Wakati wa kustaafu kwake kutoka timu ya England mwaka 1970, alikuwa ameichezea timu ya Taifa mechi nyingi kuliko mchezaji yeyote (mara 106 katika ngazi ya juu) ila Wayne Rooney kaivunja kwa mechi 107, kwa aliyocheza  mwaka jana dhidi ya Uswisi. Rekodi hii tangu wakati huo ilikuwa kwa upande wa Bobby Moore na Peter Shilton. Aliondoka Manchester United na kuwa meneja wa Preston North End katika msimu wa 1973-1974. Ambapo alikuwa mchezaji-meneja na baadaye kuwa mkurugenzi wa Wigan Athletic, Msimu uliofuata akawa mwanachama wa bodi ya wakurugenzi Manchester United tangu mwaka 1984 mpaka sasa msimu wa 2016/17.


Huyu ndiye Sir Robert "Bobby" Charlton aliyeshikilia rekodi ya ufungaji wa mabao Uingereza kwa miaka 47, HAPPY BIRTHDAY LEGEND!



Unakaribishwa kuacha comment yako hapo chini!

HIP HOP: HII NI NGOMA MPYA YA INTERNATIONAL RAPPER BENYSOFAR-WE LIKE PARTYING

Fanya uwezalo kusapoti "talent" hii ya Benysofar.



Unakaribishwa kuacha comment yako hapo chini!

HIP HOP: HI NI VIDEO MSANII KWELI MC FT TODO ONE-MEMORY


                                             Video hii unaweza kuiangalia na kuipakua hapa  
             
                       

                        Unakaribishwa  kuacha comment yako hapo chini kwa kile ulichokiona!

KINDA WA MIAKA KUMI ALA MKATABA JUVE

Kinda Rasheed Al Hajjawi
Mabingwa hao wa Italia, Juventus wamemchukua “kinda”  mpalestina Rasheed Al Hajjawi mwenye miaka 10, baada ya kuzungumzwa sana kwenye “media: za kiarabu siku za karibuni.   Licha ya kukulia mjini Gaza, “kinda” huyo alizaliwa na kukulia Norway.

Habari za kunaswa kwa kinda huyo zimekuja baada ya “skauti ya kisasa” ya kunyaka matukio, habari na vipaji ya mtandao wa kijamii kupitia Youtube, huku wakibashiri kuwa ni Lionel Messi mpya. ndani ya wiki ya karibuni  siku ya Jumanne pia kumetokea dogo mwingine kwa jina la Karamoko Dembele mwenye miaka 13, aliyefanya "appearance"  kwa dakika 10 za mwisho kwenye mechi ya Celtic U20's katika ushindi wa goli 3-1 dhidi ya Hearts.

Dembele akiingia uwanjani 

DOGO SI WA MCHEZOMCHEZO
Kweli si wa mchezomchezo kabla ya kutua alishaibuka kwenye mazoezi ya klabu ya Liverpool, na pia kuwa karibu na mastaa wa Real Madrid.
Dogo Rasheed akiwa Liverpool

Kwenye mtandao wa “facebook”  dogo kazitundika picha za mastaa kadhaa aliopiga nao stori.

 
Dogo akiwa na kocha wa Real Madrid, Zinedine Zidane