Tuesday 27 September 2016

BONGO KUAPISHWA LEO


Bwana Ali Bongo
Rais  wa  Gabon  Bwana  Ali  Bongo  Ondimba  anataraji  kuapishwa  leo usiku wa jumanne  kushika   hatamu  ya  uongozi  wa  nchi  hiyo  ya  Afrika  magharibi  kwa  muhula  wa  pili  baada  ya  kumshinda  mpinzani  wake  Bwana  Jean  Ping kufuatia  uamuzi  wa  mahakama  ya  kikatiba  nchini  humo  kutupilia  mbali  shauri  la  upinzani  la  kutaka  kura  zihesabiwe  upya  jumamosi  iliyopita.
Jumuiya  ya  kimataifa  imelaani uamuzi  huo  wa  mahakama  kwa  kushindwa  kufanya  kazi  kwa  uhuru  na  usawa  ambapo  akijibu  tuhuma  hizo  rais  wa  Gabon  Bwana  Ali  Bongo  Ondimba  alikuwa  na  machache  ya  kusema ‘’Jumuiya  ya  kimataifa  haikuja  kupiga  kura  hapa  bali  watu  wa  Gabon  ndio  waliofanya  hivyo  nami  nawajibika  kwa  ajili  yao’’

Taarifa  kutoka  ndani  ya  ofisi  ya  rais  nchini  humo  inadai  kuwa  hafla  ya  kuapishwa  kwa  Bwana  Ali  Bongo  itafanyika  jumanne  hii  mjini  Libreville  nchini  humo  lakini  haijaweka  wazi  ni  muda  gani  hasa  tukio  hilo  litafanyika.

No comments:

Post a Comment